Brazil imefikisha vifo 70,000 kutokana na virusi vya corona jana Ijumaa,
wizara ya afya imesema, licha ya kuwa idadi ya vifo kwa siku inaonekana
kuimarika.
Wizara imesema kumekuwa na maambukizi mapya kwa watu 45,000
na vifo1,200 katika masaa 24 yaliyopita, na kufikisha idadi jumla ya
kesi milioni 1.8 pamoja na vifo 70,400.
Brazil nchi yenye wakaazi
milioni 212, ni ya pili kuathirika vibaya na janga la maambukizi ya
virusi vya corona duniani baada ya Marekani.
Idadi ya watu waliofariki
imeongezeka mara dufu katika siku 35 zilizopita ambapo majimbo ya Sao
Paulo na Rio de Janeiro yameathirika zaidi, yote kwa pamoja yakiripoti
vifo 17,400 na 11,200.
DW SWAHILI,
0 Comments