BIASHARA YA CHUPA ZA PLASTIKI FURSA KWA VIJANA

 

📌AMISA AMIRI & WILSON JOHN.

WATANZANIA wametakiwa kubadilisha mtazamo hasi kuhusu watu wanaojishughulisha na shughuli za uokotaji wa chupa za plastiki na kuchukulia shughuli hiyo kama fursa ya kujipatia kipato cha kuendesha maisha na kukuza uchumi.

Kauli hiyo imetolewa Jijini Dodoma na Mnunuzi wa chupa za plastiki Bi. Khadija Zuber wakati akizungumza na CPC Blog ambapo amesema watu wengi wamekuwa na mitazamo tofauti tofauti kuhusu biashara ya chupa za plastiki wengi wakiwachukulia kama wahuni au vibaka

 Amesema jamii inatakiwa kuwa na mwamko juu ya biashara ya chupa za plastiki kwani ni ajira isiyokuwa na mtaji na ni rahisi kujipatia kipato.

Mimi ni mfanyabiashara ambaye najihusisha na biashara ya chupa za plastiki katika mtaa huu wa Majengo ambapo tunanunua chupa hizi na kuzipeleka kiwandani kwa ajili ya uchakataji na zikishachakatwa tunapata bidhaa mbalimbali kama majagi, nguo za tetroni, na bidhaa nyingine nyingi

Niiombe jamii na serikali kwa ujumla kwani tumekuwa tukihangaika kupata eneo la kudumu ili kuendesha biashara hizi, na jamii iamke sasa kwani biashara hii inasaidia hata majumbani kutunza mazingira kwani inasaidia kuweka mazingira safi na salama

Khadija 

Kwa upande wake muokota machupa James Andrew amesema amekuwa akipambana na changamoto nyingi katika uokotaji wake ikiwemo kudharauliwa, kutukanwa na jua kali wakati wa kuzunguka mitaani pia amesema changamoto nyingine ni bei kuwa ndogo ya ununuzi ambapo kilo moja ya chupa ni sh.mia mbili (200)  hivyo haikidhi mahitaji

Tunaomba serikali na wanunuzi kuthamini kazi yetu, waone ni jinsi gani tunakumbana na changamoto katika kutafuta chupa  ambapo serikali ikithamini na kuona mchango wa hii kazi  katika usafi wa mazingira

Marighafi hii inasaidia kupata bidhaa kadha wa kadha hivyo tunaomba jamii kwa ujumla watambue umuhimu wetu na mchango wetu katika  upatikanaji wa hizi bidhaa kama vyombo vya plastiki, chupa za maji na nguo  

Andrew




Post a Comment

0 Comments