Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa unaoendelea jijini Dodoma
wamempitisha kwa kishindo kupitia kura za ndiyo Rais Dkt. John Pombe
Magufuli kuwa mgombea urais kwa awamu ya pili kwenye Uchaguzi Mkuu
unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu 2020.
Wajumbe
wote 1,822 walioshiriki mkutano huo jijini Dodoma leo Julai 11, 2020
wamempigia Dkt. Magufuli kura za ndiyo ikiwa ni ushindi wa asilimia 100.
Hivyo,kwa mara nyingine Dkt.Magufuli ataingia
ulingoni kupambana na Wanachama wa watakaochaguliwa na Vyama vingine vya
Upinzani kusaka ridhaa ya Watanzania kuwaongoza katika nafasi ya Urais.
0 Comments