'CORONA ILIWAOGOPESHA WAJAWAZITO KUTOKWENDA KLINIKI'



📌HAMIDA RAMADHANI 

VIONGOZI mbalimbali na makundi maalumu Mkoani Dodoma wamekutana na kuazimia kwa kauli moja kuwa chachu katika kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa kuwapeleka wajawazito Kliniki.
Makundi hayo yaliyojumuisha waelimishaji kutoka sekta ya Afya,wajasiriamali wadogo wadogo,viongozi wadini na waganga wa tiba mbadala wamekutana kwa lengo la kuhamasisha jamii kuwapeleka wajawazito na watoto wachanga Kliniki ili kupunguza vifo vifo vinavyoweza kuepukika
John Yuda ni mwezeshaji na Mratibu wa mpango wa Taifa wa huduma za Afya mashuleni amesema Kutokana na kuibuka kwa mlipuko wa virusi vya Corona umeleta athari nyingi kwenye sekta mbalimbali ikiwemo ya afya ambapo imepelekea wamama wajawazito kutohudhuria Kliniki

Kwa upande wake Mratibu wa huduma za mama na mtoto Mkoa wa Dodoma Nice Mosha amesema kutokana na virusi vya Corona watu walikuwa wakiogopana huku wengine kutoona umuhimu wa kwenda Kliniki ambapo kumekuwepo na athari za kiafya kwa mama na Mtoto kutokana na kutokufata huduma za afya
Nao baadhi ya washiriki akiwemo kiongozi wa Kanisa la Rehoboth Mchungaji Edward Mbwambo na Rahel Moleli ambaye ni Muhudumu wa afya ngazi ya Jamii wao wameahidi kwenda kutekeleza maadhimio walioadhimia kikamilifu

Post a Comment

0 Comments