EWURA YAKAA MGUU SAWA HUPATIKANAJI MAFUTA WAKATI WA UCHAGUZI

Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na MAJI (EWURA) Titus Kaguo akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) akitolea ufafanuzi kuhusu kuadimika kwa mafuta nchini.



NA RAMADHAN HASSAN

MAMLAKA ya Uthibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imejipanga kuhakikisha kwamba mafuta yanapatikana kwa wingi wakati wa kipindi cha  uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu ambapo  meli mbili zinatarajia kuingiza mafuta mwezi ujao.

Pia,imesema kwamba sababu ya kuadimika kwa mafuta ni kutokana na janga la ugonjwa wa Corona ambapo kwa sasa mambo yamekaa vizuri na mafuta yatapatikana kwa wingi.

Hayo yamelezwa Jijini hapa na Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka hiyo,Titus Kaguo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini hapa.

Kaguo amesema  Ewura imejipanga kuhakikisha kwamba mafuta yanapatikana katika kipindi cha uchaguzi wa Oktoba mwaka huu.

Meneja huyo amesema Juni mwaka huu  matumizi ya mafuta yalipanda kwa asilimia  7% na Julai yakapanda kwa asilimia 12 kutokana na ugonjwa wa Corona.

“Moja ya kazi ya Ewura ni kuhakikisha wakati wa kampeni mafuta yanapatikana kwahiyo mtu yoyote ambaye ataingia hapa katikati na kuingilia biashara ya mafuta huyo ana malengo ya kuvuruga uchaguzi na sisi hatutakubali.Na adhabu kubwa ni kukufuta leseni”

Kama kuna mfanyabishara anafanya visivyo tutamchukulia hatua kali,lakini  meli ya dharua iliingia tarehe 13 mwezi wa saba ilikuwa na lita milioni 28 lakini pia kati ya 27 mwezi huu na tarehe 3 mwezi wa nane itaingia meli yenye mafuta ya lita milioni 89 ambazo hizo kwa mahitaji ya kawaida yanaweza kwenda kwa siku 20.
Titus Kaguo 

Amesema pia tarehe 10 mwezi wa nane itaingia meli yenye ujazo wa mafuta lita  milioni 67 kuziba pengo ambalo limeonekana.

“Pia Mamlaka inayoingiza mafuta nchini tumeiagiza mwezi wa nane iingize meli mbili za mafuta na hii  tunafanya kwa kuwa tunaenda katika mchakato wa kampeni na uchaguzi ili wakati huo kuwe kuna mafuta.

Amesema Ewura  imechunguza na kugundua kwamba kuna baadhi ya wafanyabiashara ambao sio waaminifu wanaficha mafuta ili waweze kupata faida.

Sasa hili tumeishaling’amua kuna eneo watu wanapiga kelele kwamba mafuta hakuna, wiki mbili kuna mtu alinipigia simu kutoka Ifakara alisema  alinunua lita moja kwa  shilingi 7000 nawaambia tutawakamata mmoja baada ya mwingine na adhabu yake atakayochukuliwa atajuta maishani

Post a Comment

0 Comments