📌NA BEN BAGO
TIMU ya Dodoma Jiji FC (DJFC) imefanikiwa kupanda Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuifunga timu ya Iringa United mabao 2:0 katika uwanja wa Jamhuri,mchezo ambao umeshuhudiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
TIMU ya Dodoma Jiji FC (DJFC) imefanikiwa kupanda Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuifunga timu ya Iringa United mabao 2:0 katika uwanja wa Jamhuri,mchezo ambao umeshuhudiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Dodoma Jiji ilihitaji
ushindi ili kujihakikishia nafasi ya kwanza katika kundi B
ambalo lilikuwa na upinzani mkali kati ya DJFC na timu ya Ihefu FC ya Mbarali
Mbeya.
DJFC na Ihefu zote zimemaliza
ligi zikiwa na alama 51 baada ya michezo 22 lakini DJFC wameongoza kundi hilo kwa utofauti
wa magoli 4 baada ya michezo ya leo ambako Ihefu wameifunga Cosmopolitan ya magoli 3:0.
Baaada ya ushindi huo
Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma ambao ndio wanamiliki timu ya DJFC amesema licha
ya wao (Jiji) kuwekeza kwenye timu hiyo lakini DJFC ni ya wana Dodoma wote hivyo
lazima wajivunie mafanikio ya timu hiyo.
Kunambi amesema
uwekezaji walioufanya msimu huu kwenye timu hiyo ni mwanzo tu wa mipango ya
jiji la Dodoma kuendeleza michezo.
Soka ni uwekezaji,huu ni mwanzo tutawekeza zaidi kuhakikisha tunakuwa na timu imara ya kupambana kwenye ligi kuu msimu ujao.
Godwin Kunambi,Mkurugenzi Dodoma Jiji
0 Comments