SERIKALI imewatoa wasiwasi wafanyabiashara
na watumiaji wa usafiri wa anga kwa kuahidi kuanza ujenzi wa Kiwanja cha
Kimataifa cha Ndege cha Msalato jijini Dodoma mara baada ya taratibu zilizobaki
kukamilika.
Akizungumza mjini humo mara baada ya
kukagua maendeleo ya upanuzi wa barabara ya kutua na kuruka ndege na sehemu ya
maegesho ya ndege Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, amesema lengo la
kutekeleza mradi huo ni kurahisisha usafirishaji kwa kuruhusu mashirika mengi
zaidi kutumia kiwanja hicho.
Niwahakikishie watanzania kuwa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato kitajengwa na kwa wakazi wa Dodoma ambao wanadai fidia, Serikali itahakikisha wanalipwa kabla ya kuanza kwa ujenzi huoNaibu Waziri Kwandikwa.
Aidha, Naibu Waziri Kwandikwa ameongeza
kuwa kukamilika kwa mradi huo kutaongeza idadi ya ndege ikiwemo ndege zenye
uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 200 kwa
wakati mmoja.
Naibu Waziri Kwandikwa ameongeza kuwa
Serikali inaendelea kuboresha usafiri wa anga nchini kwa kuendelea na miradi
mikubwa ya uboreshaji wa viwanja vya ndege zaidi ya kumi na moja nchi nzima
vikiwemo vya Lindi, Songea, Shinyanga, Musoma, Songwe na Mtwara.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa,
akizungumza na wataalam wa Kampuni ya CHICCO inayotekeleza mradi wa upanuzi wa
kiwanja cha ndege cha Dodoma, wakati Naibu Waziri huyo alipokagua maendeleo ya upanuzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege na sehemu ya
maegesho ya ndege.
Kwa upande wake Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Leonard Chimagu, amesema mradi umefikia zaidi ya asilimia 70 na kuahidi kuendelea kumsimamia mkandarasi ili kuhakikisha viwango vinazingatiwa.
Mhandisi Chimwangu, ameongeza kuwa kwa sasa
kazi zinazoendelea na ni kuweka tabaka la pili la barabara ya kuruka na kutua
ndege mara baada ya tabaka la kwanza la kushindilia mawe kukamilika.
Naye Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha
Dodoma, Bi Bertha Bankwa, amesema kuwa kukamilika kwa upanuzi wa sehemu ya
maegesho ya ndege utaruhusu ndege zaidi ya nne kupaki kwa wakati ikiwemo ndege
kubwa ya AIRBUS.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, akitoa
maelekezo kwa Meneja wa Ujenzi na Matengenezo
kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Mhandisi Focus Kadeghe, alipokagua maendeleo ya upanuzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege na sehemu ya maegesho
ya ndege katika kiwanja cha ndege cha Dodoma.
Mradi wa upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha
Dodoma, unafanywa na Kampuni ya CHICCO, na unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti
mwaka huu na utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 3.5.
0 Comments