KURA ZA MAONI MPWAPWA: MADIWANI 7 WASHINDWA TETEA KATA ZAO,RUSHWA YATAJWA



📌NA MWANDISHI WETU

Baadhi ya Wagombea wa nafasi udiwani viti maluum kupitia Jumuiya ya Wanawake wa Chama cha Maapinduzi (UWT) wilaya ya Mpwapwa wamelalamikia vitendo vya Rushwa kutawala katika uchaguzi hizo.

Mmoja wa Watia Nia katika nafasi ya  Udiwani viti maluum ambae hakutaka jina lake kufahamike amesema  baadhi ya wagombea wametumia fedha kuwanunulia chakula na vinywaji  Wajumbe ili waweze kuchaguliwa.

Kufuatia kura hizo za maoni zilizofanyika katika viwanja vya CCM wilaya hapa,Chama Cha Mapinduzi kimepata wagombea wanaotarajiwa kupambana na vyama vingine vya siasa katika uchaguzi Mkuu mwishoni mwa mwezi Oktoba ili kupanda masiwani watakao unda baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya Mpwapwa.

 Baraza hilo litakuwa na  Madiwani 46 wakiwamo 33 Madiwani wa Kata na Madiwani 13 viti maluum kutoka katika Tarafa zote za Wilaya ya Mpwapwa.

Mmoja wa wagombea Grolia Manyemba Tarafa ya Kibakwe akionyesha namba yake ya kura kwa Wajumbe hawapo pichani.


Waliongoza kura za maoni ni Nelly Kaguri,(429)  Shani Bilali (306)Rehema Vahaye (300) na Mariam Makasi (263)

Wakati majina mengine ni Juliana Ninde (296)Nowadia Lumambo (372) na Dorisia Fweda (200) Sophia Chidalamai (371)  na  Maria  Kigosi  kura 391.

Wengine ni Grolia Manyemba 290,Zelly Ngowo 232,Frida Nyoka na Rehema Mtinangi 248.
Aidha Madiwani  3 wameshidwa  wakitete nafasi zao  na kujikuta Wajumbe wakiwatoa nje ya mfumo ambao ni Devota Samweli, Pamela Mnemele, na Teresia Wolle.

Wakati Madiwani wa 7 waliweza kutetea nafasi zao na kurudi tena kwenye kinyang'anyiro. Msimanizi wa uchaguzi huo bwana Henry Mwenge Katibu Mwenezi mkoa wa Dodoma amesema huo ni mchakato wa awali na kuwataka wagombea kuwa watulivu wakisubiri maamuzi ya vikao.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa uchaguzi wa wilaya ya Mpwapw Jackson Shiluh amesema kuhusu vitendo vya Rushwa kama kuna mgombea ana ushahidi wa tuhuma wanazo zitoa,wapeleke ofisini na yatasikilizwa na kufanyiwa kazi malalamiko hayo.

Naye mkuu wa wilaya ya Mpwapwa bwana Jabir Shekimweri amewataka wagombea udiwani wazalendo katika kutetea maslahi mapana ya Kata zao wilaya na Taifa kwa ujumla.

Post a Comment

0 Comments