MAGUFULI KUPEWA TUZO KABLA YA KUMALIZA MUDA WAKE.KISA... MKONGE!!!



NA HAMIDA RAMADHANI

MKUU wa Mkoa wa Singida Dkt.Rehema Nchimbi amesema, wanatarajia kumpa tuzo Rais Dk,John Magufuli kwa kuinua zao la Mkonge hapa nchini kabla ya kumaliza kipindi chake cha pili cha uongozi.
Dkt.Nchimbi ameongea hayo leo katika kikao cha wadau wa zao la Mkonge kilichofanyika Jijini hapa, ambapo kwa kauli moja walikubaliana kuweka mikakati wezeshi kwa kwa ajili ya kuinua zao hilo kurudi kama zamani.

Nasema hivi sisi tutampa tuzo ya kuinua zao la mkonge hapa nchini Rais Dk,John Magufuli kabla muda wake wa uongozi kumalizika, kwani tuna kila sababu ya kufanya hivyo 
Dkt.Nchimbi.

Aidha Dkt.Nchimbi amesema kuwa kama mambo makubwa ambayo hayakuwezekana kufanyika katika kipindi kifupi cha utawala wake Rais Magufuli yamefanyika kwanini zao la Mkonge ishindikane wakati kuna kila kitu kinachohitaji kukuza zao hilo.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa, zao la Mkonge miaka ya nyuma ndio lilikuwa linaongoza kwa kuliongezea Taifa mapato, hivyo watahakikisha wanatumia mbinu zilezile kulirudisha zao hilo katika chati hapa nchini.

‘’Kipindi cha nyuma zao la mkonge lilikuwa linaongoza kwa kuliongezea mapato Taifa kwa asilimia 65, hivyo mkakati uliopo sasa ni kulirudisha  zao hilo na kushika nafasi ya kwanza katika uzalishaji hapa nchini’’, amesema Mkuu huyo wa Mkoa wa Singida.

Aidha nchimbi amesema katika utawala huu wa Magufuli mambo ambayo yalidhaniwa hayawezekani lakini yamewezekana hivyo Mkuu huyo amesema Mungu huyo huyo aliyemuwezesha Magufuli kuufanya Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi, ndiyo huyo huyo atakayesaidia kufufua zao la Mkonge hapa nchini.

Unajua hapa Dodoma ndio madhabau ya Rais Magufuli ambaye alimuomba Mungu yakafanyika mambo makubwa katika muda mfupi, sasa na sisi tutumie madhabau hiyo hiyo kukufufua za la Mkonge
Dkt.Nchimbi.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Mkonge Saad Kambona amesema kuwa wameweka mkakati ya kuinua zao hilo kwa kuwashawishi Wakulima wadogo kulima zao hilo ili uzalishaji uongezeke kwa kasi.

‘’Unajua baadhi ya watu wanafikiri kilimo cha Mkonge kinafanywa na Wakulima wakubwa tu, siyo kweli, hata wakulima wadogowadogo wakifanya kilimo hicho kwa wingi uzalishaji utakuwa mkubwa na Serikali itaongeza pato la Taifa’’, amesema Kambona.

Mkurugenzi huyo amesema kuwa hivi sasa wanazalisha tani 36,000  tu, lakini mkakati uliopo ni kuzalisha tani 120  hadi 150 kwa mwaka na inawezekana Kambona alitoa mfano wa  Brazil ambayo ndiyo inaongoza kwa kilimo cha Mkonge kwa kuzalisha tani 150 hadi 200 ambao Wakulima wadogo ndiyo wanazalisha kwa wingi zao hilo, ikifuatiwa na Tanzania ambayobado inasuasusa.

Hivi karibuni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameenda Tanga kuunda Bodi mpya ya Mkonge  na kurudisha baadhi ya mali na mashamba ya Bodi ya Mkonge zilizokuwa zimetaifishwa na baadhi ya mafisadi.

Naye Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba amesema serikaliina mpango wa kuinua zao la mkonge hapa nchini ili kuhakiisha linafikia malengo waliojiwekea.

Amesema haitakuwa tayari kuona waliopewa viwanda wanaviatamia badala ya kuviendeleza ili kuwasaidia wakulima wamkonge hapa nchini.

Serikali haitakuwa tayari kuwavumilia wenye viwanda ambavyo hawavifanyii kazi,tayari nimemuagiza Msajili Hazina aanze kuwasaka wanaoatamia viwanda
Mgumba.

Post a Comment

0 Comments