MILIONI 874 ZATENGWA KUWAENDELEZA WABUNIFU





NA HAMIDA RAMADHANI

NAIBU Waziri wa Elimu ,Sayansi na Teknolojia  Willam ole Nasha amesema kuwa katika mwaka wa fedha 2020/2021 serikali imetenga kiasi cha shilingi milioni 874 kwa ajili ya kuwaendeleza wabunifu nchini.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dodoma na naibu waziri  huyo wakati wa hafla ya kutunuku vyeti na zawadi kwa washindi wa mashindano ya kitaifa ya sayansi teknolojia na ubunifu (MAKISATU) 2020.

Ole Nasha amesema  ili kuendeleza bidhaa ziweze kufikia kwenye kiwango cha kuingia sokoni na kutumika na watanzania na walaji wengine serikali haina budi kutenga kiasi hicho cha fedha.

Aidha amesema kutokaana na jitihada za serikali za kukuza na kuwaendeleza wabunifiu wachanga nchini inakadiriwa kuwa vijana elfu 15 wamepata ajira zisizo rasmi na vijana 600 wamepata ajira rasmi kupitia masuala ya ubunifu sayansi na teknolojia.

Kwa upande wake naibu katibu mkuu wa wizara hiyo Profesa James Mdoe  amesema MAKISATU ni moja ya mikakati ya serikali ya kuibua,kutambua na kuendeleza ubunifu na ugunduzi unaofanywa na watanzania hususa ni wale wa hali ya chini.

Nao baadhi ya wadhamini wa mashindano hayo wameishukuru serikali kupitia kwa wizara ya elimu,sayansi na teknolojia kwa kuanzisha mashindano hayo yenye tija katika kuiendeleza serikali ya viwanda na hivyo kuwaomba wadau wengine kujitokeza kudhamini.

Mashindano ya makisatu yalianzishwa rasmi mwaka 2019 na wabunifu mahiri 60 walitambuliwa ambapo wapo katika hatua mbalimbali za kuendelezwa huku serikali kupitia wizara ya elimu ilitoa kiasi cha milion 750 kwa ajili ya kuendeleza ubunifu na teknolojia za wabunifu hao ili ziweze kubiashararishwa na hivyo kutumika kutatua changamoto mbalimbali katika jamii.

Post a Comment

0 Comments