NGALYA ATESA KURA ZA MAONI KATA YA KIZOTA


📌NA BARNABAS KISENGI

Aliyekuwa diwani wa Kata ya Kizota jijini Dodoma kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jamali Ngalya ameongoza katika kura za maoni zilizofanyika katika Kata hiyo.

Ngalya ambaye ametia nia kutetea kiti chake katika kata hiyo maarufu jijini hapa amepata kura 94 kati ya kura 112 kutoka kwa wajimbe wa mkutano mkuu wa kata hiyo.

Mtia nia Bakari Juma ameshika nafasi ya pili baada ya kupata kura 17 akifuatiwa na Peter Ngamangira aliyepata kura 1.

Post a Comment

0 Comments