TAARIFA
iliyotolewa na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango,
imeeleza kuwa Mhe. Rais, Dk. John Pombe Joseph Magufuli kwa jitihada kubwa za
kukuza uchumi wa nchi umeiwezesha Tanzania kuingia kwenye nchi za kipato cha
kati miaka 5 kabla ya lengo lililoweka kwenye Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025.
Mheshimiwa Dkt. Mpango alifafanua kuwa
Dira ya Taifa ya Maendeleo ya Mwaka 2025 inatekelezwa kupitia mipango ya
maendeleo ya miaka mitano mitano ambapo Mpango wa Kwanza wa Maendeleo
ulitekelezwa kuanzia mwaka 2011/12 - 2015/16 ambao ulikuwa na dhima ya
kufungulia fursa fiche za maendeleo na Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa
Miaka Mitano 2016/17 - 2020/21 una dhima ya kujenga uchumi wa viwanda ili
kuchochea mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya watu.
Kwa mujibu wa Benki ya Dunia Tanzania,
ni miongoni mwa nchi tatu duniani zilizopanda na kuingia kwenye kundi la nchi
za kipato cha kati kwa kundi la chini mwaka 2020. Nchi nyingine ni Benin na
Nepal.
Katika Afrika kundi hili kwa sasa lina nchi
22, yaani Angola, Algeria, Kenya, Benin, Senegal, Lesotho, Tanzania, Cameroon,
Tunisia, Comoros, Congo, Ivory Coast, Morocco Gibout, Egypt, Zambia, Eswatini,
Nigeria, Zimbabwe, Ghana na Cape Verde.
Kigezo muhimu kinachotumiwa na Benki hiyo kuzitambua nchi zenye uchumi wa kati ni wastani wa Pato la Mwananchi (Per Capita GNI).Dkt. Mpango
Nchi zenye uchumi wa kati huwa na
wastani wa pato la taifa la kiwango cha kati ya dola za Marekani 1,036 (sh.
2,391, 088) hadi dola za Marekani 4,045 (sh. 9,335,860) kwa kundi la chini na
dola za Marekani 4,046 hadi dola za Marekani 12,535 kundi la juu. Vigezo vingine ni pamoja na kasi ya ukuaji wa
uchumi, mfumuko wa bei na viwango vya kubadilishia fedha.
Alisema hatua hiyo iliyofikiwa ina
manufaa mengi, yakiwemo kuongezeka kwa wigo wa upatikanaji wa fedha za mikopo
ya kibiashara kwa ajili ya miradi ya maendeleo, kuvutia uwekezaji, kuwa na
uhuru wa kupanga matumizi na kuondokana na kadhia ya utegemezi.
Alimshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. John
Pombe Joseph Magufuli, wadau mbalimbali wakiwemo wakulima, wavuvi, wafugaji,
wafanyabiashara, wachimbaji wa madini, mabenki na wananchi wote kwa ujumla kwa
mchango wao mkubwa ulioiwezesha nchi kufikia mafanikio haya
Aidha, aliwashukuru viongozi wenzake
katika Wizara ya Fedha na Mipango na Benki Kuu ya Tanzania kwa jitihada kubwa
za kusimamia uchumi kulikowezesha mafanikio haya makubwa.
Pia ninaona fahari kwamba historia hii
imeandikwa wakati nikiwa Waziri wa Fedha na Mipango.
Nimezungumza na Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kuhusu tukio hili na amefurahishwa sana kwa mafanikio haya makubwa na anawapongeza Watanzania wote kwa ushindi huu mkubwaDkt. Mpango.
Imetolewa na
Benny Mwaipaja
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedfa na Mipango
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedfa na Mipango
0 Comments