UKWELI KUHUSU LUSINDE 'KIBAJAJI' KUKAMATWA NA TAKUKURU KWA TUHUMA ZA RUSHWA





NA HAMIDA RAMADHANI

TAASISI  ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Dodoma imethibitisha kuwahoji  wabunge wawili wa chama cha Mapinduzi CCM Livistong Lusinde na Peter Selukamba na  kuwachunguza  kutokana na kile kinachodaiwa na kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Selukamba amekamatwa eneola Dodoma Hoteli jijini hapa akitaka kuwapa rushwa wajumbe wa NEC,na wapiga kura wake,huku Lusinde akikamatwa nyumbani kwake akigawa rushwa kwa wapiga kura wake.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Takukuru mkoani Dodoma Sosthenes Kibwengo alisema Takukuru Dodoma inaendelea na uchunguzi dhidi ya watu hao,ilihali tayari awali wamekutwa na viashiria vya vitendo hivyo vya rushwa ambavyo ni kinyume na sheria ya Takukuru.

Ni kweli tumewakamata wabunge hao na Takukuru inaendelea na uchunguzi kwa ajili ya kuhakikisha ukweli wa suala hilo unajulikana.
Kibwengo.

Kibwengo amesema kwa upande wa Lusinde inadawa kugawa fedha kwa wajumbe wa NEC CCM nyumbani kwake, huku mwenzake amekutwa na kashfa hiyo katika maeneo ya Dodoma hoteli.

Amesema taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zilieleza kuwa mapema Julai 7,2020 kupitia kwa wasamaria wa jimbo la Mtera, Livingston Lusinde (Kibajaji) amekamatwa na Takukuru na kuwekwa chini ya ulinzi pamoja na kusitisha mkutano wake na wajumbe wa CCM.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa imekuwa ni kawaida yake kuwaita wapiga kura wake na kuwaandalia chakula na baadaye kuwapatia fedha kila ifikapo kipindi cha uchaguzi.

Kibwengo amesema julai 7,2020 Takukuru ilipokea taarifa kutoka katika chanzo chake kuwa Mbunge huyo anagawa fedha kwa wajumbe nyumbani kwake, ambapo baada ya maofisa wa taasisi hiyo kufika nyumbani hapo waliwakuta wajumbe wa CCM takribani 20.

Amesema licha ya kuwakuta wajumbe hao hawakukuta wakigawiwa fedha kama taarifa zilivyoeleza isipokuwa walikuwa wameandaliwa chakula.

“Tuliwashikilia kwa muda hapo nyumbani kwake kwa ajili ya kuwahoji, ambapo wao walijitetea kuwa wajumbe hao walifika kumsalimia mtu amejifungua nyumbani hapo, lakini kama tunavyojua ukienda kumsalimia aliyejifungua kuwezi kwenda bila zawadi lakini wao hawakwenda na chochote,” alisema Kibwengo na kuongeza.

“Siwezi kuzungumza zaidi kwani bado uchunguzi wetu unaendela dhidi ya tuhuma hizo kwa lengo la kupata ukweli zaidi, lakini niwakumbushe wananchi wote kuwa rushwa haikubaliki na hatuwezi kuwafumbia macho wanaojihusisha na vitendo vya kutoa au kupoke rushwa,” amesema.

Kwa upande wake mbunge wa jimbo hilo Livingston Lusinde akizungumzia tuhuma hizo amesema hajakamatwa na rushwa kama ambavyo taarifa zinasambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Hizo taarifa sio za kweli na mimi nimeziona kwenye mitandao ya kijamii, ni za uzushi tu.
Lusinde.

Mbunge huyo ambaye ameongoza nafasi hiyo kwa awamu mbili mfufulizo kuanzia mwaka 2010 anatajwa kuwa ni miongoni mwa watakaoomba ridhaa ya chama kugombea nafasi hiyo katika jimbo hilo.

Mbunge huyo anakuwa wa kwanza katika mkoa wa Dodoma kuchunguzwa na Takukuru kutokana na kudaiwa kujihusisha na rushwa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.

Kwa upande wa Selukamba na naye amekutwa na tuhuma kama hiyo hiyo ya kutaka kutoa rushwa.TAKUKURU imetoa wito kwa watia nia na wagombea kujihadhari na vitendo vya rushwa kwa kuwa taasisi  hiyo imejipanga kukomesha vitendo vya rushwa katika chaguzi.

Post a Comment

0 Comments