WAFANYAKAZI WA MAJUMBANI WALILIA MKATABA NAMABA 189



📌NA HAMIDA RAMADHANI
WAFANYAKAZI wa Majumbani na Mahotelini wameiomba Serikali kuridhia na kupitisha Mkataba namba 189 ili uwasaidie kupata haki zao za msingi kama wafanyakazi wa kada zingine .
Hayo yamebainishwa leo jijini Dodoma hapa katika warsha ya kikosi kazi cha kuendeleza mikakati ya kuridhia Mkataba namba 189 iliyofamnyika katika ukumbi wa Maktaba .
Wakiongea na Waandishi wa Habari wafanyakazi hao wa majumbani wamesema kuwa kama Serikali itapitisha mkataba huo wafanyakazi wa ndani na mahotelini watakuwa na nguvu ya kudai haki zao za msingi kama wafanyakazi wengine.
Akiongea kwa niaba ya wafanyakazi wenzake Sarah Mwasandube amesema kuwa wafanyakazi wa ndani wamekuwa wakidharaulika huku wakionekana kama watu maskini hali iliyopelekea hadi kwenda kutumikishwa kazi hizo majumbani.
Amesema kutokana na dhana hiyo waajiri wengi wamekuwa wakiwanyanyasa kwa kuwapiga,kuwabaka, kuwalawiti na wengine kuwanyima  mishahara yao.
Mkataba huu ukipitishwa wafanyakazi wa majumbani na mahotelini tutakuwa na nguvu katika kutetea haki zetu kwa nguvu kubwa.
Sarah Mwasandube
 Aidha,amesema kama mkataba huo utapitishwa pia utakuwa nyenzo imara kwa chama cha kutetea haki za wafanyakazi wa majumbani (CODAWU) kuwasaidia katika kuhakikisha wanapata haki zao.
Naye Dorisia Waziri ambaye pia ni mfanyakazi wa ndani amesema kundi hilo linahitajika kupata haki zote kama mfanyakazi mwengine ikiwemo bima ya afya,kuchangia mifuko ya hifadhi ya jamii kwa ajili ya kujiwekea mafao yake ya uzeeni au kuacha kazi lakini hayo yote yamekuwa tofauti kutokana na kutokuwepo kwa muongozo wa mkataba huo.
Kwa upande Mratibu wa masuala ya Kijinsia kutoka Shirika la Kazi  Duniani (ILO) Chiku Semfuko amesema mkataba huo ni mzuri na  umesimamia kazi zenye staha,ambapo mfanyakazi anatakiwa afanye kazi sehemu salama.
Naye Michael Sabuni kutoka Dawati la Jinsia  la Jeashi la Polisi Wilaya ya Dodoma amesema kuwa wamekuwa wakipokea kesi nyingi za wafanyakazi wa majumbani kwa kufanyiwa ukatili ukiwemo hule wa kiuchumi .
Malalamiko mengi tunayoyapokea ni tabia za waajiri kuwakata wafanyakazi wa ndani makato mbalimbali ikiwemo yale ya hifadhi ya jamii lakini waajiri hawapeleki pesa hizo.
Michael Sabuni


Post a Comment

0 Comments