Waganga Wafawidhi wa hospitali wote nchini
wametakiwa kujijengea uwezo wa kujitegemea katika kuboresha huduma za afya
nchini kwa kuwa wabunifu katika huduma na vyanzo vya mapato ili kupunguza
utegemezi wa kifedha toka Serikalini.
Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi
mara baada ya kutembelea hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma katika ziara yake
ya kujionea hali ya utoaji huduma za afya zinazofanywa na hospitali za rufaa za
mikoa.
Mjenge mfumo wa kujitegemea kwani mnapaswa mambo mengine kuyafanya wenyewe katika kuendesha hospitali zenu licha ya serikali kuwapatia fedha
Amesema licha ya serikali kuwapatia fedha
ni wakati sasa kuondoa mtazamo huo kwani serikali itawasaidia masuala kadhaa
hivyo mambo mengine lazima wajitegemee ili kuacha kulalamika na kutoa huduma
mbovu kwenye hospitali hizo
Hatahivyo amewataka waganga wafawidhi kukaa
na watumishi wote kuweza kupata mawazo ambayo wanaweza kuboresha Hospitali zao
na kuweza kuongeza vyanzo vya mapato na kutoa motisha kwa wafanyakazi wake.
Kwa upande kwa huduma za kibingwa Prof.
Makubi alielekeza viongozi wa hospitali hizo zishirikishe watumishi na jamii katika kuboresha hali ya
utoaji huduma katika maeneo yao.
Hata hivyo Prof. Makubi ametoa miezi mitatu kwa waganga wafawidhi
wote wasiokua wabunifu waamke na kuahidi wizara yake itafanya tathmini na kuchuja Waganga wafawidhi wanaoendana na
kasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wale ambao wataonekana
hawafai wataondolewa.
WAMJW-Dodoma,
WAMJW-Dodoma,
0 Comments