📌BEN BAGO
JAMII imetakiwa kuwakumbuka Wanafunzi wenye mahitaji maalumu ili kutengeneza mazingira rafiki kwa wanafunzi hao kumudu msomo yao.
JAMII imetakiwa kuwakumbuka Wanafunzi wenye mahitaji maalumu ili kutengeneza mazingira rafiki kwa wanafunzi hao kumudu msomo yao.
Wakizungumza baada ya
kugawa msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo vyakula kwa wanafunzi wa Shule ya
Msingi Buigiri Wasioona iliyopo Wilaya ya Chamwino,wana Jumuiya ya Walimu
Wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOSTA) wamesema jamii inapaswa
kukumbuka kundi hilo la wanafunzi ili waweze
kumudu masomo yao.
Mwenyekiti wa Jumuiya
hiyo Gerald Kwagilwa amesema licha ya wao kupeleka vyakula na mahitaji mengine
wamegundua kuwa hata idadi ya walimu katika shule haitoshelezi mahitaji.
Katika Chuo Kikuu cha Dodoma kinatoa ‘program’ ya elimu ya mahitaji maalumu lakini walimu wanamaliza na hawana ajira.
Kwagila ameiomba
serikali kuajiri walimu hao ili kuziba upungufu wa walimu hao katika vituo vya
wanafunzi wenye uhitaji maalum.
Naye mweka hazina wa Jumuiya hiyo Mwalimu Teddy Gilosa amesema wameamua kutoa msaada huo wa vitu
mbalimbali shuleni hapo ikiwa ni sehemu ya mpango wao wa kila mwaka
kurudisha tabasamu kwa jamii.
Mwalimu Teddy amesema
licha ya wanachama wa jumuiya hiyo kuchangishana ili kupata pesa za kununua
mahitaji hayo kwa watoto lakini Chama Cha Walimu Tanzania nacho kimewaunga
mkono katika kutimiza zoezi hilo.
UDOSTA mlezi wetu ni CWT,hivyo nao wametusaidia kwa kiasi kikubwa kupata mahitaji haya ambayo leo tumewaletea watoto hawa
Mwl.Teddy Gilosa
Kwa upande wake
Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo,Sospeter Jonathan amewaomba wadau kuendelea
kujitokeza kuwasaidia wanafunzi katika mahitaji mbalimbali ikiwemo uboreshwaji
wa miundo mbinu shuleni hapo.
Mwalimu Sospeter
amesema miundo mbinu iliyopo siyo rafiki kwa wanafunzi wasioona japo anasema
haiwazuii wao kutotimiza majukumu yao.
Njia(barabara) wanazotumia wanafunzi wetu wasioona sio nzuri na huwa zinaharibika sana kipindi cha masika hivyo inakuwa vigumu kufika madarasani
Shule ya Msingi ya
Buigiri Wasioona ina milikiwa na Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Central
Mashariki na inaendeshwa kwa ushirikiano wa Kanisa hilo na Serikali.
0 Comments