WANADODOMA TUENDELEE KUWA WATULIVU-RC MAHENGE



📌NA DEVOTHA SONGORWA

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Binilith Mahenge  amewataka wakazi wa Mkoa  huo  kuendelea kuwa watulivu wakati huu ambapo Taifa lipo katika maeombolezo ya siku saba kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa. 
Dk. Mahenge amesema hayo wakati viongozi mbalimbali wa serikali wakitoa heshima zao za mwisho zoezi ambalo linafanyika kwa siku tatu kuanzia jumapili iliyopita likitarajiwa kukamilika leo jumanne  katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.
Amesema kwamba katika uongozi wake alikuwa na mchango mkubwa katika Mkoa wa Dodoma pamoja na nchi nzima kwa kuanzisha Mamlaka na Taasisi mbalimbali kwa lengo la kulipatia Taifa maendeleo.
“Tutaendelea kuenzi vision aliyoianzisha alipambana kadri anavyoweza akiwa madarakani kwa kugusa kila sekta naamini alitamani kuona Tanzania inakuwa tofauti ikiwa mikononi mwake hakuwa msiri alipenda sana uwazi na ukweli hata ukikosea hakunyamaza kwa sababu alitaka kuona kila mmoja anatenda kadri ya majukumu yake kw anafasi anayoitumikia tumepoteza mtu muhimu sana”alisema Mkuuu wa mkoa wa hapa.
Akizungumzia uanzishwaji wa TASAF aliongeza “Marehemu Mkapa yeye ndiye aliyeanzisha Programu za TASAF tulikuwa na Tasaf ya kwanza, ya pili na sasa tuna ya tatu kwa sababu hakuwa tayari kuona wananchi wanaishi katika hali ya umasikini uliokithiri na ni moja ya vita ya Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kupiga vita maradhi, ujinga na umasikini na alitembea katika nyayo hizo na sasa tunaona Kaya nyingi masikini walau wanamudu mahitaji yao ya msingi”aliongeza Dk. Mahenge.
Amebainisha kwamba mengine amabyo atakumbukwa kwayo ni kuanzisha Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)
Aidha ameeleza kwamba wakati wa uhai wake ,Mkapa atakumbukwa kwa mfumuko wa bei za bidhaa kutokupanda mara kwa mara, migomo ya vyombo vya usafiri wa umma na kuwahimiza watu kufanya kwa kazi kwa bidii akiesema mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe.
Katika nyanja ya tasnia ya habari aliweka bayana kwamba katika utendaji wake hakuiacha tasnia hiyo muhimu kwa nchi akipambana kutetea uhuru wa vyombo vya habari ambapo katika uongozi wake kulifunguliwa vyombo vya habari ambavyo hutumika kama daraja la maendeleo ka taifa lolote lile duniani.
“Tusisahau kwenye vyombo vya habari yeye  kama mwanahabari na msomi alileta mageuzi makubwa sana alitetea uhuru wa habari hata kuanzishwa kwa TV nyingi zilianzshwa katika utawala wake mimi nilikuwa nje ya nchi kwenye masomo yangu lakini nilishuhudia mambo makuba aliyoyafanya hatutamsahau”alihitimisha Dk. Mahenge.
Hayati Benjamini William Mkapa alizaliwa Novemba 12, 1938 mkoani Mtwara na alifariki usiku wa kuamkia julai 24 mwaka huu baada ya kupata mshutuko wa Moyo wakati akipatiwa matibabu  ya maradhi yalkiyokuwa yakimsumbua jijini Dar es salaam.
Amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za kisiasa na uongozi ikiwemo Urais kwa Awamu ya Tatu kuanzisha Novemba 23 1995 hadi Desemba 2005 alipong’atuka madarakani. Wakati wote huo alikuwa pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)


Post a Comment

0 Comments