DC SHEKIMWERI AAMURU MWENYEKITI KUKAMATWA,KISA?SHAMBA LA BANGI



📌NA BARNABAS KISENGI

MKUU wa Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma Jabir Shekimweri amemuagiza Mkuu wa Polisi wilaya hiyo (OCD) kuwakamata viongozi wa kijiji cha Kibodiani wilayani hapo kwa kushindwa kumkamata kijana wa kijiji hicho kwa tuhuma za kulima bangi.

Kijana huyo ambaye jina lake halikuweza kutambulika mara moja anatuhumiwa kulima bangi  zaidi ya ekari moja katika eneo la milima ya kijiji hicho.

Akiongozana na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya katika ziara ya kutembelea maeneo hayo.Shekimweri aliamuru shamba hilo litekeketezwe baada ya kubainika uwepo wa mihadarati hiyo.

Shekimweri baada ya kuliteketeza shamba hilo, amemuagiza Mkuu huyo wa  Polisi  kuhakisha anamkamata mwenyekiti wa kijiji hicho na viongozi wengine kwa uzembe na kutobaini uwepo wa shamba hilo.

DC Shekimweri amesema viongozi hao watawajibika kwa kumlinda kijana huyo na kutanabaisha kwamba shamba hilo lipo karibu na barabara wanayopita viongozi hao wa kijiji kila siku na wakiwa wanaiona lakini wamefumba macho.

Serikali ipo na ina mkono mrefu kwa wale watakao kuwa wanajishughulisha na kilimo cha bangi, watakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya dola na kuchukuliwa hatua kali kwa mujibu wa sheria.
Jabir Shekimweri

Aidha,Shekimweri  amewataka wananchi wa Mpwapwa kuhakikisha wanafanya kampeni kwa ustarabu na kuzingatia maelekezo yaliyotolewa na Tume ya Uchaguzi na kuwaonya watakaoleta vurugu kwamba watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Post a Comment

0 Comments