WANAWAKE WASHAURIWA KUCHAGUA VIONGOZI WATAKAO WAUNGANISHA NA DUNIA.



📌NA DOTTO KWILASA
KUELEKEA uchaguzi mkuu unaotarajiwa kuanza Oktoba 28 mwaka huu,wanawake wametakiwa kujitoa kuwachagua viongozi Wenye maono ya kuwaunganisha wanawake  na dunia.
Wito huo umetolewa  na wanawake wajasirimali  Katika Jukwaa la "Mwanamke Shujaa Tanzania"  linaloendelea Katika uwanja wa kumbukumbu ya mwalimu Nyerere"Nyerere Square"jijini Dodoma. 
Mwenyekiti wa Jukwaa  hilo mkoa wa Dodoma Peris Privatus  amesema ikiwa wanawake watakubali kushiriki kikamilifu Katika uchaguzi mkuu wataweza kuchagua na kuwapa nafasi viongozi wenye ndoto za kuwaingiza wanawake katika uchumi wa viwanda na kuwasaidia kujikwamua kiuchumi bila kutegemea kuwezeshwa na wanaume.
Pamoja na hayo Mwenyekiti huyo wa Mwanamke Shujaa ameongeza kuwa ili kufika kilele cha mafanikio kwa pamoja,wanawake wanapaswa kusaidiana kuzifikia ndoto za kila mwanamke mmoja mmoja.
Wanawake  wajasiriamali   tuna nafasi kubwa katika jamii yetu ya Tanzania na Dunia nzima kwa ujumla,tuna wajibu wa kuwahamasisha wanawake wenzetu kujituma na kukubali mafanikio;Kwa kuanza ,tumeleta bidhaa zetu hapa kuonyesha wanawake wenzetu kuwa ni Wakati wa mafanikio ya wanawake na dunia,hakuna kubaki nyuma.
Peris Privatus 
Kwa upande wake Katibu wa Jukwaa hilo la Mwanamke Shujaa Dodoma,Emeryciana Mbulagwisha alisema ingawa baadhi ya wanawake wengi hawajapata ujasiri wa kuishi kufuatana na  matakwa yao, wapo wengine wanaoishi na kutimiza ndoto zao katika maisha yao kila siku.
Katika mafanikio ya kila mwanamke tunahimiza   nguvu ya mwanamke katika jamii tukiamini wanawake wote wanaweza  kuchukua nafasi hii kutambua ujasiri na upambanaji wao katika jamii
Emeryciana Mbulagwisha

Licha ya hayo aliongeza kuwa Jukwaa la Mwanamke Shujaa Katika karne hii, lingependa kuona kila mwanamke anapewa kipaumbele  na kuwezeshwa katika jamii, jambo litakalosababisha wanawake wengi kujitambua na kufanya mambo makubwa zaidi na kutambulika kimataifa.

Mwanamke mpambanaji ni mwanamke imara na anayeijua nguvu iliyo ndani yake ya kupambana na kukabiliana na changamoto katika nyanja mbalimbali za  maisha ili kutimiza malengo yake
Emeryciana Mbulagwisha
Tumaini Kyando ni mmoja wa wajasirimali Mwanamke Katika Jukwaa hilo ambapo amesema kuwa licha ya wanawake kukabiliana na changamoto nyingi wanapaswa kuongeza juhudi bila kuchoka kupambana.
Kyando aliongeza kuwa ,ili kuwa na wanawake wengi mashujaa lazima kuongeza zaidi  ujasiri katika nafasi za kujiendeleza na kuinuana bila kuoneana wivu wa maendeleo . 
Naye Several Joseph ametumia nafasi hiyo kuwaaminisha wanawake kwa kusema kuwa mwanamke jasiri haogopi kushindwa na  changamoto zilizo mbele yake, siku zote huchagua kuzikabili. 
Amesema,Wanawake wengi wajasiri wamefanikiwa kuinua uchumi wao na kuzisimamia familia zao, wakati mwingine bila hata ya msaada wa mwanaume.
Kila Mwanamke mpambanaji ana ndoto za kuwa mtu fulani ama kufikia malengo fulani,hivyo basi hatupaswi kuogopa kuwa tofauti na mategemeo ya wengine
 Several Joseph

Post a Comment

0 Comments