JUMUIYA YA WAHANDISI SEPTEMBA 3 WANA ‘JAMBO LAO’ DODOMA




📌NA HAMIDA RAMADHANI

JUMUIYA ya Wahandisi Tanzania inatarajia kuadhimisha siku ya Wahandisi kwa Mara ya 17 September 3 hadi 4, 2020 tokea kuanzishwa  kwake jijini Dodoma .

Aidha katika maadhimisho hayo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa  Katibu Mkuu Kiongozi Balozi,Mhandisi, John Kijazi.

Akiongea na waandishi wa Habari Leo jijini hapa Msajili bodi ya usajili wa Wahandisi  Patrick Barozi amesema malengo makubwa ya kuadhimisha siku ya Wahandisi ni kuiwezesha Jumuiya ya kihandisi kuonyesha Umma nini Wahandisi wa Tanzania wanaiweza kufanya katika kuleta maendeleo ya nchi.

Malengo kuwawezesha Umma kutambua michango tunu  inayofanywa  na Wahandisi wa Tanzania katika maendeleo ya kijani na kiuchumi nchi.
Mhandisi Barozi.


Na kuongeza kusema kuwa"Kuwawezesha  waajiri wa Wahandisi na watumiaji wa huduma  za kihandisi kutambua uwezo wa Wahandisi wazalendo na kampuni za ushauri wa kihandisi za kizalendo" amesema

SHUGHULI ZITAKAZOFANYWA SIKU YA WAHANDISI

Amesema katika siku hiyo shughuli mbalimbali zitafanyika ikiwemo Kongamano la Wahandisi vijana,majadiliano ya kitaaluma,kiapo Cha Wahandisi wataalama, Maonesho mbalimbali ya ubunifu,teknolojia na biashara, kutoa tuzo mbalimbali kwa Wahandisi na makampuni yalioshamiri kwenye sekta ya uhandisi na kuwatambua na kuwazawadia Wahandisi wahitimu walioufanya vizuri zaidi katiaka mitihani yao ya mwaka wa mwisho 2019 na 2020.

Kwa upande wake Profesa Bakari  Mwinyiwiwa Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi amesema moja ya Shughuli  ni kukagua miradi na kuona kama ina kiwango au ipo chini ya kiwango.

Aidha amesema kwa muda wa miaka mitano jumla ya Wahandisi 264 waliofanya kazi zisizo na kiwango wamechukuliwa hatua za kisheria na watakao kula kiapo siku hiyo ni  5050.

Post a Comment

0 Comments