MAVUNDE:MITANO ILIYOPITA NILIKUWA NAJIFUNZA NIPENI MITANO TENA NIFANYE MAAJABU





📌NA.FAUSTINE GIMU GALAFONI
MGOMBEA Ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM)Jimbo la Dodoma Mjini  Anthony Mavunde amewaomba  wananchi kumpa kura ili aweze kuongoza tena kwa kipindi cha miaka mitano (5) mingine kwani miaka mitano iliyokwisha alikuwa anajifunza .
Mavunde amesema hayo katika mkutano wa Kampeni uliokuwa unafanyika kata ya Ihumwa jijini Dodoma ambapo amebainisha kuwa endapo atachaguliwa kuwa kiongozi atafanya maajabu katika jimbo hilo.


Nataka niwahakikishie DUWASA  2020/2021 wamepanga bajeti kuhakikisha maji yanasambaa  katika eneo lote la kata ya Ihumwa,miaka mitano niliyokuwa naongoza nilikuwa najifunza vile.
Anthony Mavunde


Aidha,Mavunde amesema amesema suala la barabara atahakikisha wanakamilisha katika kata hiyo endapo atachaguliwa tena.
Barabara Mhe.Rais aliahidi barabara tunahakikisha mkituchagua tena tunakamilisha ,pia umeme tutahakikisha unaenea maeneo yote 34 yaliyobaki
Anthony Mavunde




Post a Comment

0 Comments