MGOGORO MSUMBIJI: WFP YASEMA RAIA WALAZIMIKA KUTOROKEA TANZANIA

 


📌BBC SWAHILI

KASKAZINI mwa Msumbiji, mapigano yanaendelea na kuongezeka hali ambayo imelazimisha maelfu ya watu kutoroka makazi yao.

Sasa hivi idadi kubwa ya raia hao wanakimbilia nchi jirani ya Tanzania kulingana na mkurugenzi wa Shirika la Chakula Duniani eneo la Kusini mwa Afrika alipozungumza na BBC.

Makadirio kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa na wadau wengine ni kwamba idadi ya kundi hilo la wakimbizi ni karibu watu 1000.

Aidha kulingana na Shirika la Chakula Duniani, sasa hivi serikali ya Tanzania ndio inayosimamia mahitaji ya kundi la wakimbizi walioingia nchini humo kutoka Msumbiji hivi majuzi.

Pia kuna taarifa kwamba unyanyasaji wa haki za binadamu katika eneo la Cabo Delgado umekuwa ukiongezeka huku mapigano kati ya wanamgambo wa Kiislamu na vikosi vya serikali yakiendelea.

Mpaka kati ya Msumbiji na Tanzania ni mto Ruvuma, na eneo la pwani ya bahari. Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, Msumbiji imeshuhudiwa idadi kubwa ya watu wakilazimika kutoroka makazi yao hasa katika mkoa wa Cabo Delgado huku wengine wakielekea eneo la kusini la Nampula, amesema mkurugenzi wa WFP.

Kulingana na Lola Castro mkurugenzi wa Shirika la Chakula Duniani eneo la Kusini mwa Afrika, wiki kadhaa zilizopita Shirika hilo lilipata taarifa kwamba kulikuwa na kundi la watu lililovuka mpaka kutoka mto Ruvuma na kuingia eneo la Mtwara nchini Tanzania.
Inasemekana kwamba baadhi ya watu walitumia boti huku wengine wakiogolea katika mto Ruvuma kuingia nchini Tanzania.

Usafiri ulizoeleka katika mto Ruvuma ni mtumbwi pia wanavuka kwa kutumia boti hadi visiwani eneo la delta la Msumbiji na Tanzania

Lola Castro.

Hatahivyo, tatizo ni kwamba wakimbizi katika eneo la Cabo Delgado na Nampula ambapo kulikuwa na watu karibu elfu 310, idadi hiyo imeongezeka pakubwa katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita.

''Hii imesababishwa na ukosefu wa usalama na mapigano ambayo yamekuwa yakiendelea. Raia wanatoroka makwao na kuacha kila kitu nyuma, na kinachotatiza zaidi ni kwamba wamekuwa wakiondoka tangu mwezi uliopita, kilele cha msimu wa mavuno

''Na kundi hilo halina chakula wakati ambapo shirika la chakula duniani limekuwa likiwapa chakula kwa karibu mwaka mmoja sasa hadi watakapoweza kurejea kwenye makazi yao na kurejelea shughuli za kilimo,'' amesema Lola Castro.

Shirika la Chakula Duniani limasema raia wa kaskazini mwa Msumbiji wamekuwa wakishuhudia ukosefu wa usalama na mapigano yamekuwa yakiendelea kwa karibu miaka mitatu, raia wameuawa, wametoroka makazi yao na sasa hivi wanakimbilia Tanzania na kuna uwezekano hali ikaendelea kuwa mbaya zaidi pengine wafanikiwe kurejea nyumbani, lakini tayari hali inatarajiwa kuwa mbaya kwa mwaka mmoja kwasababu msimu mwingine wa mavuno unatarajiwa kuwa miezi ya Machi, Aprili na Mei mwaka ujao

  BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

 


Post a Comment

0 Comments