MGOMBEA UDIWANI AFARIKI,KATIBU CCM ASIMULIA CHANZO


📌NA NOEL STIVIN

MGOMBEA Udiwani kata ya Mlembule  kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)  wilayani Mpwapwa  Wilson Mgunga amefariki dunia.

Kwa mujibu wa Katibu wa CCM wilaya ya Mpwapwa Jackson Shilluah amesema Mgombea huyo amefariki usiku wa kuamkia tarehe 02 Septemba 2020  katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma (General) alipokuwa akipatiwa matibabu .

Shilluah amesema Mgunga alikuwa diwani wa kata ya Mlumbule kwa awamu mbili mfululizo na aliteuliwa na CCM na kupitishwa na Tume ya Uchaguzi kugombea awamu ya tatu katika uchaguzi wa mwaka huu.

Taarifa kamili ya chanzo cha kifo chake waganga (Daktari) wake wanaweza wakawa nazo ila tunajua chanzo cha kuanza kuugua ambapo alipata ajali ya pikipiki ambapo Mgunga akiendesha pikipiki aligonga gari aina ya Noah na  alivunjika miguu, mkono pamoja na mbavu tatu.
Jackson Shilluah


Msimamizi wa  wa uchaguzi  wa wilaya ya Mpwapwa Sweya Mamba  amesema kwa mujibu wa Sheria, kanuni na taratibu za Tume ya Taifa ya Uchaguzi zinataka  kusitishwa kwa uchaguzi katika eneo hilo ambalo mgombea aliyepitishwa amefariki  na utafanyika  ndani ya siku 30 baada ya uchaguzi.

Aidha Bwana Sweya amesema tayari ameshatuma taarifa hizo Tume ya Uchaguzi na kuwataarifu vyama vyote kusitisha kwa zoezi la Kampeni katika kata hiyo kwa nafasi ya udiwani  na hadi hapo  Tume itakapo toa maelekezo mengine.

Post a Comment

0 Comments