MSIMAMO WA TUME YA UCHAGUZI KUHUSU TUHUMA ZA LISSU DHIDI YA JPM



📌NA DOTTO KWILASA

TUME ya Taifa ya uchaguzi (NEC)imeandaa daftari la huduma ya wapiga kura lenye wapiga kura wapatao 29,188,347 na vituo vya kupigia kura vipatavyo 80,155.

 Mkurugenzi wa Tume hiyo Dk.Wilson Charles Mahera alisema hayo wakati akitoa taarifa kwa umma juu ya maandalizi ya uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu.

Amesema kwa sasa tume hiyo inashughulika   na kuratibu kampeni za uchaguzi kwa na manunuzi   na usambazaji wa vifaa vya kupigia kura katika majimbo mbalimbali nchini .

Licha ya hayo Mkurugenzi huyo amesema tume hiyo imeelekeza nguvu katika kutoa elimu ya mpiga kura ikiwa ni pamoja na kuandaa maandalizi ya kuwateua wasimamizi wa vituo vya kupigia kura.

Katika hatua nyingine Tume hiyo imekanusha taarifa zilizoenezwa kwenye mitandao ya kijamii zikimtuhumu  Rais John Magufuli kufanya kikao na Wakurugenzi na wasimamizi wa uchaguzi mjini Dodoma.

Amefafanua tuhuma hizo,Dk.Mahera amesema taarifa hizo ni za uongo ,uzushi na zenye kuleta taharuki miongoni mwa watanzania na wapiga kura na kujenga picha kuwa uchaguzi mkuu hautakuwa huru na haki na kwamba hata wakishindwa kihalali basi watataka watanzania wawaunge mkono kuvuruga amani kwa ajenda zao binafsi.

“Tangu tarehe 25.09.2020 na 26.09.2020 tunaendelea na ziara ya kukagua na kuratibu maandalizi ya uchaguzi katika majimbo ya mikoa ya manyara ,Arusha na Kilimanjaro na mikoa mingine na kote nilikopita nimekutana na wasimamizi wa uchaguzi katika maeneo yao ya kazi,

Na katika hili niudhihirishie Umma wa watanzania kuwa taarifa zilizotolewa na Tundu Lissu zinalenga kuvuruga amani jambo ambalo halikubaliki hivyo kwa mamlaka ya kisheria niliyonayo ya Tume ya uchaguzi tayari nimemwandikia Lissu barua ya kumwita katika kamati ya kikao cha maadili cha kitaifa aje kujielezakwa Ushahidi

 Dk.Mahera.

Pamoja na hayo NEC inawataka wagombea wa vyama vyote kufuata sheria ,kanuni na taratibu za nchi ili kulinda amani katika kipindi cha kampeni za uchaguzi kilichobaki kwa kujali muda wa kampeni ,ratiba na kuepuka matusi ,tuhuma zisizo na Ushahidi zenye lengo la kuwadanganya watanzania kuwapa kura za huruma.

Post a Comment

0 Comments