NDEJEMBI AANZA MAPAMBANO YA 'KIJIJI KWA KIJIJI'

 


📌NA BARNABAS KISENGI

MGOMBEA ubunge Jimbo la Chamwino mkoani Dodoma Deogratus Ndejembi kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ameanza kampeni ya kuomba kura za Rais, Mbunge na Madiwani kwa mikutano ya  kata kwa kata, kijiji kwa kijiji na kitongoji kwa kitongoji katika Jimbo la Chamwino mkoani Dodoma.

Mgombea huyo ambaye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa  ameanza kampeni yakeya kijiji kwa kijiji kwa kukutana na makundi maalum ya wajasaliamali wakiwemo bodaboda na mamalishe katika Kata ya Haneti kijiji cha Izava na Segeli .

Nimeanza kukutana na makundi haya ndiyo yanajumuisha watu wengi na pia wanachangamoto nyingi  hivyo ni lazima nikutane nao na kuweka mikakati ya kuwainua kiuchumi na kutatua changamoto zinazowakabili kwa kipindi  cha miaka mitano (5) watakachonichagua.

 Deogratus Ndejembi



Pia Ndejembi amesema kama wananchi watamchagua kuwa mbunge atahakikisha Jimbo hilo linakuwa la mfano kwa maendeleo katika mkoa wa Dodoma.

Mgombea huyo amefafanua kwamba kutokana na uwepo wa makazi ya Rais wa Tanzania jimboni hapo panahitaji mtu mwenye uwezo kusukuma maendeleo kuendana na kasi ya maendeleo katika eneo hilo na mkoa wa Dodoma.



Ziara hiyo ateendelea nayo kwa kuhakikisha anaongea na makundi yotekatika Jimbo hilo lenye Kata kumi na 14 za Jimbo hilo la chamwino



Post a Comment

0 Comments