SELIKALI YAPOKEA GAWIO KUTOKA AIRTEL


📌NA DOTTO KWILASA.
SERIKALI kupitia Wizara  ya fedha na Mipango imepokea jumla ya shilingi bilioni 32.9 ikiwa ni gawio kutoka kwa kampuni ya mawasiliano ya Airtel Tanzania.
Kati ya fedha  hizo, shilingi bilioni 18.99 ni gawio huku bilioni 14 ikitolewa na kampuni hiyo  Kama sehemu ya  zawadi yake katika kuchangia  shughuli za maendeleo.
Akipokea Gawio hilo kutoka kwa Airtel Tanzania, Katibu Mkuu Wizara ya fedha na mipango, Dotto James amesema kiasi hicho cha gawio kitasaidia katika kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo ya nchi.
Amesema katika historia ya uwekezaji wa serikali katika kampuni zenye uwekezaji wa hisa chache kiasi hicho hakijawahi kufikiwa na mwekezaji yeyote huku akiongeza kwamba bodi na menejimenti ya Airtel Tanzania iendelee kufanya kazi kwa bidi ii kuepuka kuingia hasara kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Airtel Tanzania,Gabriel Malata mesema kuwa hivi sasa ubia baina ya Serikali na Kampuni hiyo umeimarika ambapo serikali inamiliki hisa asilimia 49huku airtel ikimiliki hisa asilima 51.

Aidha amesema hisa hizo zimeongezeka kutoka asilimia 40 na kwamba hayo ni mafanikio makubwa kwa Serikali na hivyo kwa sasa Serikali kupitia msajili wa hazina itakuwa inapata gawio la bilioni18.99  kwa mwaka.

Hata hivyo amesema kuwa utekelezaji huo umeenda sambamba kuhakikisha wabia wanapata gawio kama walivyokubaliana ikiwa ni pamoja na kutoa mchango wa bilioni 14 kama mchango wa maendeleo.


Pia kampuni hiyo imekuwa ikijihusisha katika huduma mbalimbali za kijamii na katika kukabiliana na virusi vya corona iliweza kuchangia kiasi cha Sh milioni 700 .

Mwenyekiti huyo amesema ili kuhakikisha malengo hayashuki ni lazima watahakikisha wanaiboresha aitel Tanzania kuwa na huduma bora zaidi ikiwa ni pamoja na kuwa na siku maalum ya airtel pamoja na kufanya tathmini nchi nzima wanapotoka,walipo na wanapokwenda.

Naye Msajili wa Hazina Athumani Mbuttuka amesema kuwa katika Kupitia utendaji na umiliki wa kampuni ambayo serikali ina hisa,katika kipindi cha miaka miwili iliyopita serikali imefanikiwa kuongeza umiliki wake katika kampuni za Airtel kutoka asilimia 40 hadi 49.

Kampuni zingine ni pamoja na Udart kutoka asilimia 49 hadi 85,Keko pharmaceuticals limited asilimia 40 hadi 70,na Mecco kutoka asilimia 2 hadi 25. 
Athumani Mbuttuka

Aidha amesema kuwa uchambuzi bado unaendelea katika kampuni nyingine kama Inflight Catering Services Limited.

"Napenda kuwaasa bodi na menejimenti ya Airtel  kutoridhika na gawio mlilolitoa kwa serikali  na wanahisa wengine bali muendelee kudhibiti matumizi huku mkiimarisha teknolojia katika utoaji wa huduma na kuhakikisha kuwa kampuni hairudi tena ilikotoka ambako kumezaa makubaliano haya tunayoyatekeleza"amesema.

Post a Comment

0 Comments