SERIKALI KUONGEZA UZALISHAJI MAZAO YANAYOTOA MAFUTA.



📌NA DOTTO KWILASA

SERIKALI imesema ipo kwenye mchakato wa kuongeza uzalishaji  wa mafuta ya kula nchini kwa mazao yote yanayotoa mafuta  ikiwemo alizeti, na michikichi  ili kuzuia kuingia kwa mafuta kutoka nje ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa  jijini hapa na Mkurugenzi wa udhibiti ubora {TBS} Lazaro  Msasalaga wakati akitoa mafunzo kwenye semina kwa wazalishaji,wasambazaji,na wauzaji wa mafuta ya kula.

Amesema lengo kubwa la serikali  ni kuzingatia mahitaji makubwa ambayo kwa sasa  wananchi wanahitaji ili  kuweza  kuzalisha mafuta ya kula kwa wingi nchini.

Waziri ana mradi mkubwa wa  kupanda michikichi kule Kigoma lengo kubwa ni kuongeza uzalishaji wa mafuta nchini, na si kwenye michikichi tu inaenda kuangalia na uzalishaji wa mazao mengine kama alizeti na namna Mkoa husika unavyoweza kuzalisha zao hilo

Lazaro  Msasalaga

Aidha amesema  katika mafunzo hayo  wamepita wilaya zote  za mkoa wa Dodoma na inarajia kwenda  Singida  ili kuweza kuwaelimisha wazalishaji na wauzaji namna ya kuyatunza mafuta ili  yawe na ubora.

“ Tumeenda kongwa kibaigwa hapa tutaenda manyoni singida tutaendelea kusambaza elimu hii japo Kuna changamoto ambazo tunazipata lakini nasi tunaziwekea mikakati  kiukweli kama mafuta yasipofungashwa vizuri kwa kupigwa na mwanga wa jua mafuta yanaweza kuharibika”

 Amesema katika mafunzo hayo wanasisitiza katika uhifadhi ndio maana wanawatembelea  wauzaji wa barabarani waweke vibanda kukinga mafuta   kwani jua linapopiga mafuta yanaharibika.

 Naye Daudi  Makala, mzalishaji mdogo wa mafuta ya alizeti amesema  amejifunza namna ya kuzingatia ubora wa mafuta  kwani kwa kufanya hivyo  atampa uhakika mtumiaji .

Pia tuhakikishe mbegu  imekomaa na usafi pamoja na utayalishaji wa mafuta haya kiukweli tumejifunza mambo mengi tukizingatia nafikiri walaji watafurahia  ,sisi wasindikaji wa mafuta inabidi sasa mara kwa mara tuwe na semina  ili tuweze kukumbushana

Daudi  Makala

Kwa upande wake Yunice Maneno muuzaji  kutoka soko la saba saba amesema kutokana na semina  amejifunza mambo mengi kutoka kwa mkulima hadi kufikia mafuta yenyewe .

“ Wakati mwingine unaweza kununua mafuta machungu  kumbe kutokana na  mkulima kukimbilia soko anaweza akakamua mafuta ambayo mbegu  haijakauka kwahyo mi niombe tu semina hizi tuzipate mara kwa mara na niwaombe wananchi watumie mafuta haya ya alizeti kwani ni mazuri kwa afya”.Amesema Yunice.

Post a Comment

0 Comments