TCIB YAZIJENGEA UWEZO ASASI ZA KIRAIA JUU YA UTEKELEZAJI WA MIKATABA WAZI KWENYE MANUNUZI YA UMMA




📌NA PENDO MANGALA

KITUO cha taarifa kwa wananchi(TCIB) kimeaanda muongozo wa kuwasaidia Wabunge katika kusimamia maamuzi mbalimbali yanayofanywa na Serikali katika utekelezaji wa miradi ya umma.

Kauli hiyo imetolewa Jijini Dodoma na Meneja mradi wa kituo  hicho,John Kitoka mara baada ya kutoa mafunzo kwa wadau mbalimbali wa masuala ya manunuzi kuhusiana na masuala ya manunuzi na  Mikataba ya Umma.

Kitoka amesema kuwa hiyo ni kutokana na utafiti mdogo waliofanya na kubaini kuwa  wabunge wengi kutojua taratibu na kanuni na Sheria za usimamizi wa manunuzi ya umma hivyo itawasaidia kuwaongezea maarifa katika kuisimamia Serikali Pamoja na kuihoji  juu ya miradi mbalimbali inayoitekeleza.

Muongozo  huu utawasaidia waheshimiwa wabunge kuwafumbua macho na kuweza kuihoji Serikali namna mbalimbali wanavyotekeleza miradi ya umma kwani wao ndio wawakilishi wa wanachi hivyo ni vizuri wananchi wakawa wanajua masuala ya maendeleo yanavyofanyika.John Kitoka

Aidha amesema kuwa pia muongozo huo utawasaidia Wabunge kuhakikisha manunuzi ya umma yanafanyika kwa kufuata taratibu za kisheria na miradi inatekelezwa kwakuzingatia sheria za manunuzi na michakato yote inayopelekea upatikanaji wa miradi na michakato na utekelezaji wake inazingatia   misingi ya uwazi na wajibikaji.



Kwa upande wake Annex  Moza ambaye ni  Afisa  Miradi wa TCIB,amesema kuwa Muongozo huo utawasaidia  kuangalia kwa jinsi gani wabunge wanaweza kuisaidia serikali kutimiza majukumu yake katika kufanya manunuzi.

Sisi kama kituo cha taarifa kwa wanachi tunaamini kwa muongozo huu tutaweza kuwapa Wabunge mbinu zaidi katika kuisimamia Serikali katika suala zima la bajeti  ili kuleta maendeo na  ufanisi

Annex Moza

Katika hatua nyingine amegusia suala la Mikataba mibovu ambapo amesema ni suala sugu katika nchi za kiafrika na hiyo ni kutokana na mifumo iliyopo ikiwepo usiri na hivyo kusababisha kuwepo kwa mikataba hiyo mibovu isiyotekelezeka na kuisababishia Serikali hasara. 

Daniel Msangya   ni mmoja wa baadhi ya wadau waliopata mafunzo kuhusiana na Mikataba  ya manunuzi Serikalini , amesema   manunuzi yanachukua sehemu kubwa ya fedha za  Serikali  hivyo ni lazima kuwepo mifumo ya wazi na imara  ili kudhibiti upotevu wa fedha nyingi za umma na Mikataba ya manunuzi lazima ifanywe kwa uwazi.



Awali akiwasilisha mada Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Tarifa kwa Wananchi (TCIB), Deus Kibamba amesema kuwa Manunuzi ya serikali yanahitaji kufanyika katika uwazi kuanzia hatua za mwanzoni kabisa kwenye kuandaa mradi, kutangaza tenda ,kutoa tenda kwa wazabuni na hata utekelezaji wa mradi ili wananchi kuwa na uelewa juu ya miradi inayotekelezwa .

Tanzania inapambana kutatua tatizo hilo ili miradi ikamilike kwa wakati, ufanisi na ubora uendane na thamani ya pesa ya mradi husika

Deus Kibamba.

 

 


Post a Comment

0 Comments