📌NA DOTTO
KWILASA
BAADHI ya Wakazi Kata ya Mtumba jijini Dodoma
wameuomba uongozi wa serikali ya mtaa huo kuwatatulia changomoto ya uhaba wa
maji ambayo imedumu kwa muda mrefu .
Aidha
wakazi hao waliopo karibu na mjini wa serikali wamesema kuwa hali hiyo inawasababisha kushindwa
kufanya shughuli zao kimaendeleo na kutumia mda mwingi kutafuta maji.
Wakiongea jana jijini hapa wananchi hao
wamesema kumekuwa na changomoto kubwa ya maji kwa kipindi cha miezi
miwili sasa.
Hagulwa Manase amesema uhaba wa maji
unawakosesha wanawake wengi kushindwa kutimiza majukumu yao kifamilia.
Muda mwingi maji yanatoka kwa nusu saa kisha yanakata,watoto wetu wanashindwa kupata huduma za malezi ,tunaomba Serikali utusaidie
Naye Pendo Manga Abraham ametumia nafasi hiyo
kuomba uongozi wa mtaa huo kuhakikisha wanatoa ratiba ya maji ili kila
mwananchi aweze kupata maji .
Kuna muda maji yanatoka wakati ambao watu hawapo majumbani kwa kuwa tumezoea maji hayatoki Sasa ukitoka unakuta maji yamekata
Pamoja na hayo amesema hapo awali maji
yalikuwa yakitoka bila kukatika na kufanya jamii ya eneo hilo kufanya shughuli
zao za uzalishaji mali bila vikwazo .
"Tunasikitika kuona hali imebadilika
ghafla baada ya maji kukatika kila wakati na kujikuta tukikosa maji,Kuna wakati
maji hayatoki kabisa kwa muda wa wiki hapo tunaanza kununua maji ya kisima kwa
Shilingi 300,"amesema.
Licha ya hayo wakazi hao wa Mtumba wameongeza
kuwa licha ya eneo hilo kuwa maarufu kutokana na kuwepo kwa ofisi nyingi
za serikali (Mji wa serikali) lakini eneo muhimu kama hilo linakuwa na
changamoto ya maji.
Kutokana na hayo Mwenyekiti wa mtaa huo Robert
Chigugude amekiri kuwepo kwa changomoto hiyo huku akisema imetokana
na kuongezeka kwa watumiaji wa huduma hiyo jambo ambalo limesababisha pampu
inayosukuma maji kushindwa kuhimili idadi ya watumiaji wa sasa.
Aidha amewataka wananchi kuwa watulivu wakati serikali ikishughulikia changamoto hiyo kwani wamepeleka taarifa kwa mamlaka ya usimamizi wa maji vijijini (RUWASA) na kwamba matengenezo yanatarajiwa kufanyika muda wowote kuanzia sasa.
Niwatoe wasiwasi wananchi wangu,naomba wawe wavumilivu kwani tuna mpango wa kusahihisha changamoto zote zinazotokana na maji
Robert Chigugude
0 Comments