WAGANGA WA TIBA ASILI 'WALIA' NA GHARAMA ZA UPIMAJI WA SAMPULI ZA DAWA



📌NA HAMIDA RAMADHANI 

UMOJA wa Wagaga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania (UWAWATA) wameiomba Serikali kupunguza gharama za upimaji wa sampuli za dawa pindi zipelekwapo kwa mkemia mkuu.

Akizungumza na waandishi wa Habari kwenye banda lao  katika Viwanja vya Nyerere Square kwenye wiki ya Tiba Asili Afrika  Mwenyekiti  wa Bodi za  dawa  za asili  kutoka UWAWATA Nurdin Lyimo amesema  kiwango cha kupima dawa ni kikubwa na gharama nyingi wanatumia mpaka kupima kutokana na wengi wao kutoka mikoani kwenda Dar es salaam .

Tunatoka mikoani tukifika pale kupima dawa ni zaidi ya laki 6 hapo na bado utatumia gharama nyingine za nyumba za kulala wageni bado hujala na unatumia zaidi ya siku mbili tatu kwahiyo mi niiombe tu Serikali kwakweli itupunguzie gharama hizi
Nurdin Lyimo

"Siyo wote wanaweza kumudu gharama hiyo  kuna wengine wana dawa nzuri kabisa lakini bei ni kubwa wanashindwa  hivi juzi tulikumbwa na janga la ugonjwa wa Corona sisi tukatengeneza dawa inayoitwa NUT  inayotibu ugonjwa huo lakini mchakato haukuwa mrefu  nadhani lilienda haraka kutokana na uzito wa ugonja lakini kiukweli mchakato ulikua mrefu" amesema 

Naye Mratibu wa Mafunzo ya kuinua Tiba  asili nchini Ally Maganyari ameiomba serikali isambaze Maabara za upimaji wa sampuli za dawa katika kila mkoa ili kuweza kupunguza msongomano.

Niiombe tu serikali yetu chini ya uongozi wa Rais wetu  Jonh Magufuli itusogezee hizi maabara kwa sababu na yeye pia amesharuhusu sisi tufanye kazi basi tunaomba na hili pia atusaidie.
Ally Maganyari 

Pia ameitaka jamii isiwe na imani potofu ya kuwa waganga ni wachawi na badala wajikite katika kuamini kwamba dawa za asili ni zinatokana na mimea ambayo inaota katika ardhi ya Tanzania.

"Tiba asili siyo uganga wala uchawi zamani enzi za mababu zetu wamekuwa wakitumia tiba asili na wanaonekana kuwa na maisha marefu na miili yenye nguvu siyo sawa na karne hii, hakuna kitu kilichoumbwa na Mungu halafu kikawa kibaya kwenye asili hakuna madhara,"amesema

Hata hivyo Maadhimisho ya siku ya Tiba Asili ya mwafrika yalianza rasmi mwaka 2003 baada ya mawaziri wa afya wa nchi wanachama wa shirika la afya duniani  kanda kuridhia kuwepo kwa sherehe hizo.


Post a Comment

0 Comments