WAGANGA WA TIBA ASILI WATAKIWA KUZINGATI SERA,SHERIA,NA KANUNI ZA AFYA



NA.FAUSTINE GIMU GALAFONI

Katibu mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya jamii,,jinsia ,Wazee na Watoto Prof.Mabula Nchembe amewataka waganga wa tiba asili hapa nchini kuzingatia sera,kanuni na taratibu za Afya huku akiwataka kuacha kutumia  vifaa ambavyo hawakupata mafunzo rasmi na ufanisi  wake .

Prof.Nchembe amebainisha hayo jijini Dodoma katika maadhimisho ya miaka 18 siku ya tiba asili ya Mwafrika ambapo pia amehimiza  Waganga wa tiba asili kuachana na matangazo yasiyofaa na kuweka mabango ovyo ovyo barabarani .

Hivyo waganga tiba asili ni vyema tukazingatia sera, taratibu ,sheria na kanuni za Wizara ya afya,hususan katika suala la uwekaji mabango ovyovyo barabara na kuweka matangazo yasiyofaa ,pia matangazo ya tiba asili katika vyombo vya habari lazima yapate kibali kutoka Baraza la Tiba Asili na tiba Mbadala.
Prof.Mabula Nchembe 


Baadhi ya wadau wa tiba za Asili na tiba Mbadala wakiwa katika maadhimisho ya miaka 18 ya tiba asili ya Mwafrika yaliyofanyika kitaifa viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.

Aidha,Prof.Nchembe amewahimiza watoa huduma wa tiba asili na tiba mbadala nchini kuhakikisha kuwa wamesajiliwa wao wenyewe,wasaidizi wao,vituo vyao vya kutolea huduma  na dawa zote zinazotumika.


Hali kadhalika,Prof.Nchembe amebainisha kuwa tangu mwaka 2017 serikali ianze  kusajili dawa za asili  kupitia Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala hadi sasa dawa thelathini(30)zimesajiliwa.

Kuhusu kuadhimisha miaka 18 ya siku  ya Tiba Asili ya Mwafrika,Prof.Nchembe amesema Tanzania imefanya mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutambua huduma ya tiba asili katika sera ya afya kuanzia mwaka 1990 na kama ilivyohuishwa mwaka 2007, kutungwa kwa sheria ya tiba asili na tiba mbadala  Na.23   ya mwaka 2002 ,Tanzania kuwa miongoni mwa nchi 46 za Afrika  zinazoadhimisha siku hii kuanzia mwaka 2003.

Mambo mengine ni pamoja na kuundwa kwa baraza la  Tiba Asili na tiba Mbadala  mwaka 2005 ,kutengenezwa kwa miongozo na kanuni mbalimbali za tiba asili  na tiba Mbadala mwaka 2005-2010 pamoja na kuanzishwa kwa mifumo rasmi ya kiutendaji  ndani ya serikali.

Kaimu msajili wa Baraza la Tiba Asili Patrick Seme  amesema baraza hilo limekuwa mstari wa mbele kusajili katika kuwasajili waganga wa tiba asili ili watambulike kisheria hali ambayo husaidia  kuondoa watoa huduma wa tiba asili wasio kuwa waaminifu.


Kwa upande wake Kaimu Mkuu Idara ya utafiti wa tiba asili  iliyo chini ya Taasisi ya ya Taifa ya utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Dkt. Vitus Nyigo amesema wakati wa janga la Corona walifanya tafiti za kukabiliana na ugonjwa huo ikiwemo mchanganyiko wa tiba lishe zikiwemo limau,tangawizi,pilipili,vitunguu maji na vitunguu vya kawaida .

Kaulimbiu ya Maadhimisho ya 18  tiba Asili ya Mwafrika ni “Miongo Miwili ya Tiba Asili Afrika 2001-2020 nchi zina mafanikio gani” ambapo kauli mbiu hiyo inakumbusha  kujitathmini tiba asili ilikotoka hadi ilipo na namna bora ya kuboresha .

Post a Comment

0 Comments