WANAWAKE WATAKIWA KUTUMIA WASAIDIZI WA KISHERIA KUPATA HAKI ZAO



📌NA HAMIDA RAMADHANI

JAMII imetakiwa kuacha uoga na badala yake imeaswa kuwatumia wasaidizi wa msaada wa kisheria hasa wanawake pale wanapo kandamizwa kwenye suala zima la haki zao za msingi.
Akizungumza na waandishi wa habari Jana,Afisa Ufuatiliaji Tathimini Hamisa Hamad  kutoka Pemba  kwenye kikao cha tathimini  amesema  lengo la kikao ni kufanya mapitio ya mambo ambayo tumeyatelekeza ndani ya mwaka.

Katika katika kikaokazi hiki  tunatekeleza mapitio tuliyoyafanya ndani ya mwaka mmoja na Kama inavyojulikana kwa  sisi upande wa Zanzibar msaada wa kisheria ulikua mgeni  kwetu kutokana na mila na desturi na dini.
Hamisa Hamad 

 Anasema Msaada wa kisheria kwa Zanzibar  ilikua ni kitu kigeni  kutokana na mila na desturi na dini lakini baada ya kufika mwaka 2007  baada ya  shirika la Legal services facility LSF)kufika ndipo wanawake 850 waliamka na kuanza kutoa taarifa za kikatili wanazo fanyiwa na wenza wao na kupatiwa msaada wa kisheria.

"Zamani kwa sisi waafrika kwa mila zetu na deaturi ilikua ni ngumu kutoka kwenda kumshitaki mwenza wao eti tu kwakukosea au kwakufanyia tendo la ukatili hali iliopelekea sisi wasaidizi wa kisheria kukosa takwimu sahihi za kuwatambua ni wanawake wangapi waliofanyiwa ukatili wa kijinsia"amesema Msaidizi wa kisheria Hamisa

Aidha amesema  katika mila  za kiafrika wanawake na watoto ndio wanaongoza kwa kufanyiwa ukatili wa kijinsia.


MAFANIKIO.
Amesema baada ya kuja kwa wasaidizi wa msaada wa kisheria wanawake wengi wamejitokeza na kuanza kudai haki zao za msingi ikiwemo kudai ardhi ,asilimia 99 ya wanzanzibar ni waislam.

 Amesema katika  dini ya kiislam imeainisha wazi mwanamke akifa anatakaiwa apewe haki zake kadhaa na mwanaume haki kadhaa lakini jambo hilo limekuwa likikiukwa  na wanaume wamekua wakiwakandamiza.

"Sasa ni vyema wanawake wote kujitokeza katika kudai haki zao kwani mwanamke ana haki zake ya kutunzwa kupewa mirathi na ikitokea umeachwa dai haki zako na kama ikitokea hata mwaume amefariki mwanamke anatakiwa apewe haki zakezote "amesema Msaidizi wa kisheria Hamisa

Naye Afisa Ufuatiliaji na Tathimini kutoka mkoani Lindi Nelson Choaji amesema kazi yao kubwa katika mkoa wa lindi ni kuhakikisha upatikanaji wa haki katika mkoa wa Lindi unapatikana.



Hata hivyo amesema kwa upande wa Lindi Legal Service Facility imekua ikiwapa nguvu wasaidizi wa kisheria kuhakikisha wanawafikia watu wote wenye changamoto  mbali mbali wanazokabiliana nazo katika jamii.

Tatizo kubwa la mikoa ya pwani kesi nyingi tunazokumbana nazo ni za wanaume kutekeleza familia zao mi nitoe wito tu kwa kina mama kuwatafuta wasaidizi wa msaada wa kisheria pindi wanapo hitaji haki zao za msingi.
 Nelson Choaji

Legal Service Facility ni Shirika lisilo la kiserikali lenye makao Makao Makuu yake jijini Dar es salaam lengo kuu la uanzishwaji wake ni kusaidia jamii kupata haki.

Post a Comment

0 Comments