WAZIRI MAJALIWA MGENI RASMI KARIBU DODOMA FESTIVAL




📌NA HAMIDA RAMADHANI 

WAZIRI  Mkuu  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Kassimu Majaliwa  anatarajia kuwa  mgeni rasmi katika tamasha la  Karibu Dodoma Festival 2020.

Akizungumza  na waandishi  wa habari katika viwanja vya Jamhuri  Mwenyekiti  wa Tamasha hilo na   msanii wa Bongo Movie  Simon Mwapagata  maarufu kama (Maduhu)   amesema Tamasha hilo la Dodoma Festival ni Tamasha la kwanza kuandaliwa likiwa na lengo la kukuza na kutangaza  mkoa na jiji la Dodoma ikiwa  ni sehemu  ya kuendeleza fikira za baba wa Taifa  Mwl Julius Kambarage  Nyerere   juu ya makao makuu pamoja na jitihada zinazofanywa na Rais Dk John Pombe  Magufuli katika kuendeleza makao makuu ya nchi. 

Tamasha la mwaka huu  litakua na maudhui ya kutoa fursa  Kwa makundi mbali mbali kutoa pongezi na shukrani kwa Rais Magufuli kwa kazi nzuri alioifanya kwenye makundi mbali mbali  ya jamii  na kwenye sekta mbali mbali ambazo zimefanya vizuri na kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii 
Simon Mwapagata. 

Ameongeza  kusema kuwa "Tunatumia jiji  la  Dodoma katika kuratibu mambo makubwa yanayounganisha taifa kwasababu Dodoma ndio makao makuu yenye kila sababu ya kufanya mambo ya kitaifa  pamoja na  makundi ya sekta mbali mbali "amesema


Aidha amesema katika kutoa fursa iliyokusudiwa Tamasha la karibu Dodoma festival  linatarajiwa kufanyika katika siku  3 kuanzia   tarehe 22 hadi 24  mwezi Oktoba 2020 ambapo wanatarajia Rais Magufuli kuja kufunga Tamasha hilo. 

Hata hivyo amesema makundi ya jamii pamoja na sekta mbali mbali zitapewa nafasi ya kutoa ushuhuda kwa mabadiliko waliyo yapata  Kwa kipindi cha miaka mitano cha uongozi wa awamu ya tano. 

"Haya ni baadhi ya makundi ambayo yamepata mabadiliko ya ushindi ndani ya awamu ya Tano,Boda boda, mama ntilie, machinga, watu wenye ulemavu,  wanafunzi  wa  vyuo, wanafunzi wa sekondari na msingi, vijana, wanawake, na wazee wafungwa walio huru  pamoja na waathirika wa madawa ya kulevya "amesema Mwapagata 

Makundi ya sekta mbali mbali yatakuwepo wakiwemo wavuvi, wakulima, wachimbaji wadogo, wajasiriamali na wafanya biashara ,wasafirishaji  wafugaji  tour operator  wasanii wa bongo movie na bongo flava, wana michezo,  na  viwanda vipya.
Simon Mwapagata.

Sambamba na hilo Mwapagata  amesema kuwa  Tamasha hilo pia litahusisha shughuli mbali mbali za kiuchumi  na kijamii  kama vile  Burudani ya wasanii, burudani  ya michezo ,makongamano ya makundi,  matembezi ya hisani  na maonesho ya wajasiriamali.

Post a Comment

0 Comments