WAFANYABIASHARA KATA YA MADUKANI WATOA YA MOYONI

 


📌NA HAMIDA RAMADHANI

 

WAFANYABIASHARA wadodowadogo ali maaarufu Kama Machinga waliopo Kata ya Madukani jijini Dodoma wameiomba serikali kuwapatia mikopo ili waweze kukuza mitaji yao.

Wameyasema hayo  Leo jijini hapa katika kampeni ya  mlango kwa mlango  duka kwa duka mtu kwa mtu inayofanywa na  Mgombea udiwani wa Kata hiyo ya Madukani Profesa Davis Mwamfupe kupitia  Chama Cha Mapinduzi (CCM). 

 Wafanyabiashara hao wamesikika wakilia na kuiomba serikali ya awamu ya tano kutatua kero yao kubwa ya kukosa mikopo katika kuendeleza biashara zao za  kila siku.

 Akiongea na waandishi wa habari  mbele ya Mgombea huyo wa Udiwani Hassan Ismail Mfanyabishara wa Viatu amesema licha ya kuendelea kufanya biashara zao changamoto yao kubwa Kama wamachinga ni mitaji.

"Licha ya kuwa tupo katika vikundi lakini suala zima la upatikanaji wa mikopo kwetu ili tuweze kukuza biashara zetu imekuwa ni tatizo hivyo basi tunaiomba serikali ituangalie na sisi wafanyabiashara wadogo na watupatie hiyo mikpo inayotolewa na Jiji letu," amesema Mfanyabishara  huyo.

 Na kuongeza kusema kuwa"Sisi tunaimani kuwa serikali yetu ya awamu ya tano ni sikivu na ndio maana hata Leo tumeweza kumuona Mgombea wetu ameweza kupita kwa kila Mfanyabishara akinadi  sera zake  tunaomba akipita akazifanyie kazi "amesema ismail

Naye Mathew Malima Mfanyabishara wa Saa ameiomba serikali kuwapatia mikopo ili waweze kupiga hatua katika ufanyaji wao wa biashara .

 Hatutaki kubaki pale pale kila siku na ndio maana tunaiomba serikali yetu sikivu itupatie mikopo na sisi wafanyabiashara ndogondogo tuweze kukuza na tuweze hata kumiliki fremu na kwakufanya hivyo tutakuwa tumekuwa na kuiingizia serikali mapato. 

Mathew Malima

 Kwa upande wake Mgombea huyo wa Udiwani Profesa Mwamfupe amesema amezipokea kero zote kikubwa ni kuomba Mungu ili aweze kushinda kwa kishindo na kuja kuzitatua kero zote za wafanyabiashara hao wa Kata ya Madukani.

 

Post a Comment

0 Comments