MRADI WA TUIMARISHE AFYA WA HPSS WAJIPANGA KUBORESHA MFUMO WA AFYA NCHINI



📌RHODA SIMBA

MRADI  wa  Tuimarishe afya wa  (HPSS) unaofadhiliwa  na Serikali ya Uswisi chini ya shirika la  Maendeleo la SDC Swiss Agency For Development and Copperation umejipanga  kuboresha mfumo mzima  wa afya nchini kwa kutekeleza  miradi mbali mbali kupitia serikali.

Hayo yamesemwa leo jijini Dodoma na  Meneja  mradi Ally Abdallah wakati akizungumza na waandishi wa habari  katika kongamano la saba  la wadau wa afya nchini( Tanzania Health Summit).

Aidha  amesema kuwa  lengo la mradi huo ni  kutekeleza miradi  ambayo italeta matokeo chanya na kuonekana katika jamii na unafanya  uboreshaji  katika mfumo wa afya, mfumo wa fedha, mfumo wa vifaa tiba, na mfumo wa upatikanaji wa dawa.

Mfano wa mifumo hiyo ni pamoja na  CHF iliyoboreshwa mfumo wa upatikanaji  wa dawa (Jazia PVS)na Mradi huu upo hapa katika maonesho ili kuchangia tija katika masuala mazima ya mfumo  wa afya nchini, kuchangia mifumo ya afya nchini, pamoja na kujifunza.

Ally Abdallah.

“Kwa kuwa kila tunachokifanya lazima kilete matokeo kwahiyo sisi tupo hapa ili kuonesha  miradi tuliyoifanya na si vinginevyo” amesema Abdallah

Amesema Mradi wa Tuimarishe Afya (HPSS,) ni mradi mkubwa na  wenye mafanikio kwani  upo  hadi kwenye ilani inayozungumzia upatikanaji wa dawa nchini.

Hata hivyo Abdallah amesema wao wamejipanga kuendelea kutoa  elimu  katika banda lao kwenye kongamano hilo  la saba la  wadau wa afya  kwani kupitia wadau hao ndipo wanapopata fursa zaidi ya kuutangaza mradi na kujitangaza kwa jamii kwa ujumla.

Post a Comment

0 Comments