RAIS WA UTPC AKUTANA NA MKUU WA MKOA WA KAGERA

 


📌MWANDISHI WETU, KAGERA

Rais wa Muungano wa klabu za Waandishi wa habari Tanzania UTPC Deogratius Nsokolo, amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Generali Marco Gaguti na kuzungumzia ushirikiano baina ya Serikali na Kagera Press Club.

Brigedia Generali Gaguti amesema ofisi yake itaendelea kutoa ushirikiano wa dhati kwa waandishi wa habari kutokana na umuhimu wa taaluma hiyo katika kusaidia maendeleo ya mkoa.

Waandishi ni muhimu sana, napenda tushirikiane na tuelezane juu ya kila kitu na pale inapotokea changamoto basi tuipatie ufumbuzi kwa pamoja.

Brigedia Generali Gaguti

Amesema yapo mambo mengi ya maendeleo ambayo yamefanyika na yanaendelea kufanyika katika Mkoa hivyo ni jukumu la waandishi kueleza juu ya changamoto na mafanikio.

Rais wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) Deogratius Nsokolo
 ( kulia) akiwa na na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Generali Marco Gaguti (kushoto) baada ya kutembelea ofisini kwake.


Kwa upande wake Rais wa UTPC amesema kwa sasa waandishi katika kila mkoa wanawajibu wa kuimarisha uhusiano na Serikali na wadau wengine bila ya kuathiri utendaji wao wa kazi na kuisaidia jamii kwa kufichua maovu na kutoa habari ambazo zitasaidia watawala kutenda mema kwa wananchi.

Aidha amemuomba mkuu wa mkoa kuanzisha utaratibu wa kukutana na waandishi wa habari walau mara moja kila mwaka ili kubadilishana mawazo lakini pia kupata fursa ya kujibu maswali mbalimbali toka kwa waandishi, ombi ambalo amelikubali.

Post a Comment

0 Comments