UCHAGUZI UTPC: NSOKOLO AIBUKA KIDEDEA TENA,DODOMA YATOA MJUMBE

 


📌NA BEN BAGO

UCHAGUZI wa Rais,Makamu wa Rais na Wajumbe wa Bodi ya Muungano wa Vialbu vya Habri nchini (UTPC) umekamilika hii leo mjini Morogoro.

Katika uchaguzi huo Deogratius Nsokolo ambaye ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Kigoma ametetea nafasi yake kwa kupata ridhaa ya wajumbe kuongoza taasisi hiyo kwa awamu ya pili. 

Deo Nsokolo akipiga kura


 
Nsokolo amepata kura 72 katika kura 83 ziliopigwa na wajumbe 83 huku mpinzani wake Edwin Soko ambaye ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mwanza akipata kura 11 pekee.

Matokeo hayo yanampa nafasi Deogratius Nsokolo kutumikia nafasi ya Urais wa UTPC kwa miaka mingine mitano kuanzia 2020-2025 ambapo awali alitumika katika nafasi hiyo mwaka 2015-2020.


MAKAMU WA RAIS

Pendo Mwakyembe akipiga kura yake


Katika nafasi ya Makamu wa Rais,Pendo Mwakiembe (Katibu-Mara Press Club) aliibuka na ushindi wa kura 65 na kumshinda mpinzani wake Lulu George (Mwenyekiti-Tanga Press Club) aliyepata kura 18

UJUMBE WA BODI YA UTPC
Sambamba nafasi hizo za juu,mfumo wa bodi ya UTPC inaundwa pia na wajumbe wengine 8 kwa uwino sawa wa jinsia.

WAGOMBEA WANAWAKE

Hadija Omar akipiga kura yake


 Walioshinda nafasi ya Ujumbe wa bodi ya UTPC ni;

1. Hadija Omar 48 (Mweka Hazina-Lindi Press Club)

2. Lilian Lucas 51(Katibu-Morogoro Press Club)

3. Salma Abdul 62 (Mweka Hazina-Tabora Press Club)

4. Paulina David 63 (Mweka Hazina-Mwanza Press Club)

Jumla ya kura zilizopigwa ni 83


WAGOMBEA WANAUME

Frank Leonard akipiga kura yake


 Walioshinda Ujumbe wa Bodi ni;

1. Mussa Yusuf 51 (Mwenyekiti-Central Press Club Dodoma)

2. Cloud Gwandu 61(Mwenyekiti Arusha Press Club)

3. Frank Leonard 64 (Mwenyekiti Iringa Press Club)

4. Abdallah Mfaume 69 (Zanzibar)

Kura zilizopigwa ni 83

Pia Bodi hiyo inaundwa na Mjumbe Mtaalamu Mshauri wa Masuala ya fedha ambapo mgombea alikuwa mmoja tu Bw. Eliazer Mafuru  na akazoa kura zote 83 za ndiyo

 

Post a Comment

0 Comments