KIKUNDI CHA CHAPAKAZI CHATOA ZAWADI YA MWAKA.

 


📌RAMADHANI HASSAN.

 

Kikundi cha kutunza na kuhifadhi  Mazingira cha (Chapakazi) cha Jijini hapa kimetoa zawadi ya mwaka mpya kwa wateja wake ambayo ni  punguzo la bei ya Miche ya matunda na vivuli lengo likiwa ni kuendelea kulifanya Jiji la Dodoma kuwa la kijani.

Hayo yameelezwa leo Jijini hapa na Mtunza Fedha  wa Kikundi hicho,Darwesh Said alipokuwa akizungumza na  Waandishi wa Habari.

Darwesh amesema kutokana na dhamira ya Kikundi hicho kuwa ni kuhakikisha Dodoma inakuwa ya kijani imetoa punguzo la asimia  20 ya miche yote inayouzwa katika eneo lao lilopo barabara ya Iringa.


Amesema Miche ya Miembe ambayo awali ilikuwa ikiuzwa kwa shilingi 5000 sasa itauzwa kwa shilingi  4000.

Darwesh amesema Miche ya Miparachichi,Michungwa,Mindimu na Milimao  iliyokuww  ikiuzwa kwa shilingi 5000 sasa itauzwa kwa shilingi 3000

Kwenye miche ya vimvuli amesema itauzwa kwa shilingi 2000 ambapo awali ilikuwa ikiuzwa kwa shilingi 3000.

Hata hivyo,Darwesh amewaahidi wakazi wa Dodoma wataendelea  kupata miche bora kutoka katika Kikundi hicho kwa mwaka ujao wa 2021.

"Kwanza tunawatakia Sikukuu njema,kikubwa tunawahamasisha kuendelea kupanda miti ili kutunza mazingira,ahadi yetu kwa wateja wetu ni tutaendelea kuhamasisha upandaji wa miti,na sisi tunawaomba Watanzania wapande miti,"amesema.

 Katika hatua nyingine,Darwesh amesema wameendelea kutoa huduma za maharusi kupiga picha katika bustani yao iliyopo barabara ya Iringa ambapo amewashauri maharusi ambao wanatarajia kufunga ndoa kufika katika eneo hilo.

 "Hapa kuna kila sehemu ya kupiga picha,bustani yetu ina ubora wa hali ya juu,watapigwa picha za kila aina hapa,"amesema.

 Pia,amesema vinapatikana vyungu vya kisasa katika eneo hilo kwa ajili ya Kupamba nyumba na maeneo mbalimbali.





 

Mwisho

Post a Comment

0 Comments