TAARIFA SAHIHI KUSAIDIA KUONDOA CHANGAMOTO YA HALI YA HEWA.

 

📌NA SALEH RAMADHANI.

IMEELEZWA kuwa taarifa sahihi za hali ya hewa zikiwafikia wachimbaji wa madini kwa wakati,zitaisaidia kukabiliana na changamotoza mabadiliko ya hali ya hewa.

Hayo yamesemwa na  Mhandisi Aron Kisaka wakati akimwakilisha katibu mkuu wa sekta ya uchukuzi katika ufunguzi wa mkutano wa wadau wa sekta ya madini unaojadili  umuhimu wa huduma za hali ya hewa.

Amesema kuwa taarifa hizo zitazisaidia mamlaka zinazohusika kupanga mipango ya kukabiliana na majanga ndani ya sekta yatokanayo na hali mbaya yahewa kama maporomoko ya udongo.

“Katika mkutano huu washiriki watapata fursa ya kufahamu faida za utumiaji wa taarifa za hali ya hewa kwa sekta ya madini”amesema.

Aeongeza kuwa matumizi ya huduma za hali ya hewa yanatarajiwa kuongeza tija,ufanisi na usalama katika shughuli zinazohusianana utafutaji,uchimbaji madini na uendeshaji wa migodi.

Awali  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya hewa Tanzania (TMA) Dk. Agnes Kijazi amesema,mamlaka ya hali ya hewa inatoa huduma mahususi kwaajili ya sekta mbalimbali nchini ikiwemo ya madini.

Amesema kuwa pamoja na elimu hiyo bado wadau wa sekta ya madini wahazitumii ipasavyo huduma hizo.

“Ni matarajio yetu kuwa wadau watapatiwa elimu ya matumizi sahihi ya huduma za hali ya hewa na huduma zitakazo patikana endapo watazitumia vyema taarifa hizo”amesema Kijazi.

Naye Mwakilishi wa Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa mamlaka ya hali ya hewa Tanzania Robert Sunday amesema madhumuni ya mkutano wa sekta ya madini na mamlaka ya hali ya hewa ni kuunganisha nguvu katika kuhakikisha kunaongeza pato la taifa na usalama wa watu na mali zao.

Mwisho.

Post a Comment

0 Comments