VIJANA MIAKA15 HADI 24 KUNDI LINALOPATA MAAMBUKIZI KWA KIASI KIKUBWA

 


📌HAMIDA RAMADHANI

IMEELEZWA kuwa kundi la Vijana kuanzia umri wa miaka 15 hadi umri wa miaka 24 ndilo kundi linalopata maambukizi kwa kasi kubwa nchini. 

Akiongea katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yaliofanyika katika viwanja vya Nyerere Square katibu Tawala Dodoma Keissy Maduka amesema takwimu zinaonyesha kuwa 

asilimia 44 la kundi la Vijana lipo kwenye hali hatarishi ya kupata maambukizi ya virus vya Ukimwi na Ukimwi.

Katibu Tawala huyo akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt Binilith Mahenge amesema katika kipindi cha miaka ya 2012 hadi 2014  Mkoa wa Dodoma  ulikuwa ni miongoni mwa  mikoa yenye maambukizi madogo kwa asilimi 2.4.

"Sasa tumeweza kuona takwimu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu inaonyesha kuwa hali ibadilika ambapo kuanzia mwaka 2015 hadi mwaka 2017 hali ya maambukizi mkoa wa Dodoma ni asilimia 5 hivyo Dodoma yetu imeweza kuingia kwenye mikoa hatarishi hakika hili ni tatizo kubwa hasa kwa Vijana wetu,"amisema Katibu Tawala Maduka.

Aidha ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Dodoma katika siku hiyo kujitokeza kwa wingi kwakupima na kutambua afya zao Mapema na kuacha uoga wa kujua afya zao kuwa kigezo cha kuhofia kufa Mapema.

Kila mmoja wetu ampime atambue afya yake kwani ukipima na ukijitambua mapema kama unamaambukizi ya virus vya Ukimwi unanafasi ya kuishi vizuri kea amani na furaha.

Keissy Maduka 

Kwa Upande wake mratibu wa Ukimwi mkoa wa Dodoma kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Abdih Ahmed amesema visababishi vya Ukimwi havitofautiani na vinginekatika bara la Afrika kuwa na wapenzi wengi,ngono zembe,kuchagia vitu vyenye ncha kali na hata ukatili wa kijinsia.



Amesema visababishi hivyo  vimechangia ongezeko kubwa la Vijana kuwa na maambukizi na kuwa na idadi kubwa la watoto yatima .

Takwimu kutoka NBS zinaonesha kuwa kuanzia mwaka 2017 Dodoma ilikuwa asilimia 5 ya maambukizi tofauti na mwaka 2013 mpaka 2014 hali ya maambukizi ilikuwa 2.9 hivyo Hali ya maambukizi Dodoma imeongezeka

Abdih Ahmed 

Akitoa ujumbe,mwakilishi kutoka  TACADS  Yeriko Kawanga amesema ukimwi bado ni tishio .

"Kwa mujibu wa takwimu zilizopo katika kila watu 100,watu wanne wana maambukizi ,hili janga la Taifa." Amesema

Amewataka wananchi waendelee kyjitojeza kupima Afya zao ili waanze kupatiwa tiba mapema.

Naye Annamary Oscar  kutoka konga Nacopha baraza la Vijana wanaishi na virus vya Ukimwi mkoa wa Dodoma amesema Furaha yao nikuona wamefanikiwa kuwarudisha jumla ya Vijana 122 kwa mwaka 2019 hadi 2020 waliokatisha matumizi ya dawa za kufubaza makali ya virus vya Ukimwi na Ukimwi ARVS.

Amesema kwa Upande wake pamoja na Vijana wengine wanaojitambua kuwa na virusi vya Ukimwi wamekuwa na afya zilizoimarika kwa kuendelea kutumia dawa hizo za kufubaza virusi vya Ukimwi ARVS.

Wasanii wakitoa burudani...


Post a Comment

0 Comments