WAADVENTISTA WAHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA YA MAKAO MAKUU YA NCHI DODOMA KUWEKEZA KATIKA TAASISI ZA ELIMU.

 


📌FAUSTINE GIMU GALAFONI.

Mkurugenzi Idara ya Elimu kanisa la Waadventista Wasabato jimbo kuu la
Kusini mwa Tanzania  Bi.Devotha Shimbe amewaasa waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato hapa nchini  kuchangamkia fursa ya Kuwekeza elimu kwa kujenga shule katika makao makuu ya nchi Dodoma ili kuwajengea zaidi maadili ya kiroho na yampendezayo Mungu Watoto wa shule za Kiadventista.

Bi.Shimbe amebainisha hayo jijini Dodoma wakati akifanya mahojiano Maalum ambapo  amesema kanisa linatambua mchango mkubwa unaofanywa na mshiriki mmoja mmoja hivyo ni muhimu washiriki wakawekeza katika suala la elimu  hali itakayosaidia kuwaandaa watoto kuwa na maaadili mema kwani elimu ya maadili ya kiadventista ni moja ya uinjilisti.

Hivyo,Bi.Shimbe amebainisha  kuwa elimu inayopatikana katika taasisi za elimu za kanisa la Waadventista Wasabato  zimejengwa zaidi katika maadili na falsafa ya msingi wa Biblia ambapo watoto huandaliwa katika maisha ya sasa na maisha ya milele.

Aidha, Mkurugenzi huyo wa  Idara ya Elimu kanisa la Waadventista Wasabato jimbo kuu la Kusini mwa Tanzania amebainisha kuwa  Union ina mpango wa kujenga Chuo kikuu katika makao makuu ya nchi Dodoma ambapo Jumla ya ekari 350 zilishapatikana kwa ajili ya ujenzi huo

 

Post a Comment

0 Comments