📌HAMIDA RAMADHANI:
WAZIRI wa Kilimo Profesa Adolf
Mkenda amesema kuwa bado kuna changamoto katika zao la Tumbaku hasa kwenye
suala zima la ushindani wa ununuzi wa zao hilo.
Waziri Mkenda ameyasema hayo leo
jijini hapa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya
kumalizika kwa kikao cha ndani na Bodi ya Tumbaku.
Amesema licha ya Bodi ya Tumbaku
kufanya vizuri katika suala zima la ushindani wa ununuzi wa zao hilo kwani liko
chini ,hivyo hawana budi kuongeza juhudi za Mazingira ya
ushindani katika soko.
Amesema Tanzania ni miongoni mwa
nchi 10 zinazolima na kuzalisha zao la Tumbaku huku changamoto kubwa ikiwa ni
kiwango kidogo cha ushindani.
"Tumbaku ni zao
linaloliingizia Taifa fedha nyingi za kigeni kwa mwaka USD Milioni 285
tofauti na mazao mengine yanayolimwa hapa Nchi ambavyo nayo
ni mazao ya kimkakati," amesema Mkenda.
" Haiwezekani Tumbaku ilimwe
Tanzania ipelekwe Nchini Zambia kule kwani Zambia inapata bei nzuri halafu
wanairudisha tena Tanzania nasisi ndio tuuze nchi za nje hapana tumechoka
Tanzania kuonekana ni shamba la bibi," amesema.
" Zao la Tumbaku litaendelea
kuwa zao namba moja la uchumi hapa Nchini Tanzanian amesema Waziri Wa Kilimo
Mkenda.
Na kuongeza kusema " Kunatabia
ya Baadhi ya wanunuzi kudai kuwa hawanunui tumbaku yote inayozalishwa nchini na
mikataba ya ununuzi ni michache kuliko tumbaku inayozalishwa
Amesema Tumbaku nyingi ya Tanzania
inayobaki inauzwa kwa makinikia (ulanguzi) na soko limehamia zambia kwa
kupeleka tumbaku ya Tanzania kwenye soko la zambia kwa magendo na kisha inarudi
tena kusafirisha kupitia bandari ya Tanzania
Pia ameitaka Bodi itoe majibu ya
kitaalamu kwa nini Hali hiyo inajitokeza na itoe sababu za Kufungwa kwa kiwanda
cha kusindika tumbaku kilichopo Morogoro
Pia amesema katika kulinusuru
soko la bidhaa hiyo Tanzania inafanya mazungumzo na mataifa ya misri na China
na indonesia Ili kununua tumbaku inayozalishwa nchini badala ya kutegemea makampuni
yanayohodhi soko la tumbaku duniani ambayo ni manne tu.
Mwisho
0 Comments