📌HAMIDA RAMADHANI
NAIBU waziri wa Maji
Maryprisca Mahundi amesema kuwa ni muhimu kwa taasisi za umma kuwa na
Baraza la wafanyakazi kwani mabaraza haya yameanzishwa kisheria kwa dhumuni la
kuishauri Serikali.
Uundwaji wa baraza la
wafanyakazi ni Agizo la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la
mwaka 1970, na ni utekelezaji wa Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na. 6 ya
mwaka 2004 Kifungu 73(1-3) kinachoelekeza juu ya kutekeleza Sera ya kuwashirikisha
Wafanyakazi katika uongozi wa pamoja.
Naibu waziri huyo
Maryprisca ameyasema hayo leo jijini hapa alipokuwa akifungua baraza la
kwanza la wafanyakazi EWURA katika ofisi zoa zilizopo Dodoma .
Amesema Baraza
la Wafanyakazi ndilo jukwaa la kisheria la majadiliano ya pamoja, kati ya
viongozi na watumishi katika utumishi wa umma, kuhusu wajibu na maslahi ya
watumishi.
Amesema madhumuni ya
kuanzishwa kwa baraza hilo la wafanyakazi nipamoja na kushauri serikali katika
ngazi za idara, taasisi na Wizara kuhusu usimamizi wa kazi na rasilimali watu,
utekelezaji wa majukumu,kulinda haki na wajibu wa waajiri na wafanyakazi, kutoa
ushauri kuhusu kujenga hali bora za kazi, maslahi ya Wafanyakazi na kusimamia
haki na ustawi katika sehemu za kazi.
Vile vile amesema Baraza
lina wajibu wa kutoa ushauri, kusimamia na kuhakikisha kuwa waajiri na
watumishi wanatambua wajibu na haki zao, pia wanazingatia maadili ya utumishi
wao ili kuleta matokeo ya utendaji wa kazi yenye tija, staha na upendo.
“Napenda kuwakumbusha kwamba Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kwa dhati, kuondoa uzembe, rushwa na vitendo vyote visivyofaa mahala pa kazi ikienda sambamba na kubana matumizi yasiyo ya lazima ili kuongeza tija. Hivyo, ni wajibu wa kila mfanyakazi wa EWURA kuhakikisha anafahamu wajibu wake mahali pa kazi,”amesema Naibu waziri huyo.
Pia kutekeleza malengo aliyopangiwa katika muda uliopangwa, vile vile kutunza mali na vifaa alivyokabidhiwa kufanyia kazi, pamoja na kufika kazini na kuondoka kwa muda uliopangwa
Aidha amesitiza
mambo machache ambayo ni muhimu, ambapo jambo la kwanza amewataka watumishi hao
kuzingatia Uwajibikaji, suala ambalo ni nguzo kuu ya Mafanikio
katika sehemu yoyote ya kazi.
Pia amewaomba kutoa
ushirikiano kwa watumishi ilikuondoa malalamiko na kuhakikisha wanashughulikia
masuala ya maendeleo kwa wakati kwa Wajumbe mnaowakilisha Wafanyakazi wote wa
EWURA.
“Hamna budi kuwa mfano
katika jambo hili la uwajibikaji na kuleta ufanisi lakini pia Katika mkutano
huu, nimeambiwa kutakuwa na mada zitakazowasilishwa kuhusu mabaraza ya
wafanyakazi na, vyama vya wafanyakazi hususani TUGHE. na Sheria ya Utumishi wa
Umma na Masuala ya nidhamu Ni imani yangu kuwa mtasikiliza na kushiriki
majadiliano ili mwisho wa siku tupate kuelewa kile kilichokusudiwa,”amesema .
Na kuongeza kusema “Ni
Matarajio yangu kwamba, kila Mjumbe wa baraza aliyeko hapa atatimiza wajibu
wake, Naamini sote tukifanya kazi zetu kwa umakini tutaweza kutoa mchango wetu
kikamilifu katika kufikia malengo ya Serikali ya awamu ya tano ya Ujenzi wa
Uchumi wa Viwanda na Katika kukamilisha azma hiyo, Watumishi wa EWURA
wanaowajibu mkubwa wa kuongeza kujituma na kuwa waadilifu,”amesema.
kwa upande wake
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi, Kaimu Mkurugenzi Mkuu, Muhandisi Godfrey
Chibulunje,amesema baraza hilo ni lakwanza tangia kuanzishwa kwa Ewura.
Amesema kuanzishwa kwa
baraza hilo ni kulenga kuongeza ufanisi na tija kwa wafanyakazi bila kusahau
utendaji kazi wao wa kila siku na majukumu ya EWURA.
0 Comments