UFUGAJI WA KISASA UNAWEZA KUBADILI MAISHA KWA ASILIMIA 70%.

 


📌SALEH RAMADHANI.

Kituo cha utafiti wa mifugoTaliri wilayani kongwa mkoani Dodoma kimebainisha kuwa endapo wafugaji watatumia mbinu bora za ufugaji wanauwezo wakujiongezea kipato kikubwa kitakachowapelekea kuishi maisha mazuri zaidi.

 Hayo yamebainishwa na kaimu mkurugenzi kituo cha utafiti wa mifugo Taliri kongwa DR.wilfred Munisi ambapo amesema kuwa wafugaji wakibadilika na kufuga kisasa wanauwezo wa kubadili maisha yao kwa asilimia 70 na kuwataka wafugaji kutembelea vituo vya utafiti wa mifugo nchini ili kujionea shughuli zinazofanyika katika Taasisi mbalimbali za utafiti ili  kuboresha mifugo yao.

"Tunafanya utafiti wa mifugo ili jamii ya kitanzania inufaike na ijipatie kipato maana ufugaji ni sehemu ya utajiri lakini jamii haitambui na sisi kama Taasisi ya utafiti hapa kongwa milango yetu ipo wazi kwa yule anayehitaji kujifunza namna ya kuboresha mifugo yake" amesema.

 Dr.munisi amesema kuwa hakuna sekta ambayo inalipa kama sekta ya ufugaji nchini huku akiwataka vijana kujishughulisha ili kuendana na kasi ya mabadiliko katika sekta ya kilimo na ufugaji.

"Hivi nyie vijana kwanini msifuge kisasa ili mnufaike na mifugo yenu mnayoihudumia huko nyumbani,sekta ya ufugaji na kilimo ni sehemu kubwa ya mafanikio lakini nyie hamtembelei vituo vya utafiti nchini ili mjifunze namna ya kuboresha mifugo yenu ya asili mnayoihudumia huko majumbani" amesema.

 Kwa upande wake Mtafiti idara ya mbuzi Christopher mtwange amebainisha kuwa mbuzi aina ya gogo white na buchosa wanauwezo wakuzaa mapacha sita hadi watatu endapo mfugaji atamtunza vizuri huku akisisitiza kuwa wanafanya Tafiti nyingi za ufugaji ili kuboresha mifugo na kuleta tija kwa wafugaji.

"Tunafanya hivi ili kuiboresha mifugo yetu ya asili na mbuzi hawa wanauwezo wa kuzaa mapacha watoto watatu mpaka watoto sita,mbuzi aina ya gogo white na buchosa wanauwezo wa kuvumilia ukame na magonjwa,pia mbuzi hao tunawatunza na tunawaongezea thamani" amesema

 Naye merchades Rutechura Afisa utafiti kutoka Tume ya taifa ya sayansi na teknolojia (COSTECH) amesema kuanzia mwaka 2010 serikali kupitia tume ya Taifa ya sayansi na Teknolojia imetumia zaidi ya shilling billion 50 kufadhili miradi ya utafiti na ubunifu nchini.

"lengo la kufadhili miradi ya utafiti na ubunifu ni kusambaza hizi tafiti kuwafikia wananchi na zaidi ya miradi ya tafiti mia moja tayari zimeshafanyika na zimewafikia wananchi, pia tunawaomba wanahabari kuhabarisha umma kuhusu tafiti zinazofanyika katika taasisi za utafiti wa mifugo na kilimo ili ziwafikie kwa wakati na wazitumie kwa manufaa yao na Taifa kwa ujumla" amesema.

 Hata hivyo Rutechura amesema kuwa wamegundua kuna mbegu nyingi za wanyama ambazo zinatakiwa kuwafikia wananchi ambapo amedai kuwa hiyo ni kazi ya waandishi wa habari kuhakikisha zinafika katika jamii ili iweze kutambua.

"Waandishi wa habari pelekeni hizi taarifa za utafiti ili umma utambue mbinu bora ambazo zitawawezesha wengi kuendana na mabadiliko ya tabia nchi,pia umma ufahamu hizi taasisi za utafiti na wazitembelee ili wajifunze namna ya kujiongezea kipato kwa kupitia sekta ya ufugaji na kilimo,pia matokeo haya tunataka yasaidie katika uchumi wa Taifa kwa sababu kila tunachofanya katika chuo cha utafiti tungependa kiwafikie wananchi na tunatumia fedha nyingi za Serikali ili zisaidie hizi teknolojia na kurahisisha maisha ya mtanzania,”amesema.

 Tume ya taifa ya sayansi na teknolojia (COSTECH)  iliandaa mafunzo ya siku mbili kwa Waandishi wa Habari wa Mikoa ya Dodoma na Singida pamoja na watafiti na kwa siku mbili  waandishi wa habari walipata fursa ya  kutembelea   miradi mbambali pamoja na watafiti  katika Kituo cha Utafiti wa Kilimo (Tari Makutupora),Taasisi ya Mifugo (Taliri Kongwa) na (Taliri Mpwapwa).

Post a Comment

0 Comments