WATAALAMU WA KISWAHILI WATETEA KUKUZA KISWAHILI



📌
DEVOTHA SONGORWA.

WATAALAMU wa lugha ya Kiswahili nchini wameiomba Serikali  nguvu katika Taasisi zinazofundisha lugha hiyo kwa wageni kama hatua ya kuendelea kukuza Kiswahili kimataifa pamoja na kuboresha sera zitakafungua mwanya wa wageni kuja kwa wingi nchini.

Akizungumza na mtandao huu Mmiliki wa Kituo cha kufundisha Kiswahili kwa wageni (LILINGA SWAHILI SCHOOL),Tunku Kyoba alisema kiswahili ni bidhaa inayohitajika kwa kiasi kikubwa katika mataifa ya nje hivyo ipo haja ya kuweka jitihada madhubuti kufanikisha hilo.

Alisema kumekuwa na mwitikio mkubwa wa raia wa kigeni kuja nchini kwa lengo la kusoma lugha ya Kiswahili ambapo  mataifa ya Marekani , Ujerumani na Uingereza yameonyesha uhitaji wa kufahamu lugha hiyo kwani hulazimika kuitumia katika utekeleza ma majukumu yao ndani nan je ya nchi.

“Wenzetu wametengeneza fursa kufanya kazi hapa kwetu na sera za Mashirika yao zinawataka kufahamu kwa kiswahili na utamaduni na wamekuwa wakija kwa wingi kujifunza tunaomba Serikali kuona namna inavyoweza kuboresha mazingira ya ufundishaji wa Kiswahili kwa ufasaha katika vituo vya Kiswahili na utamaduni tukidhi mahitaji yao kuongeza thamani ya lugha yetu,”alisema Kyoba.

Kyoba alisema changamoto wanazokabiliwa nazo kwa sasa ni uwepo wa ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na Virusi vya Corona kwa baadhi ya mataifa ya nje hivyo kusababisha kupungua kwa wanafunzi na mabadiliko ya sera ya Nchi kuhusu wageni katika nyanja ya utolewaji wa vibali vya makazi na kikazi.

Kwa upande wake Profesa Mshiriki katika taaluma za Kiswahili Aldin Mutembei aliwataka watanzania kubadilika kifikra kwa kutodharau lugha yao wakiamini  kuzungumza lugha za kigeni ndiyo kuelimika huku akiwahimiza wazazi na walezi kuwajenga watoto wao kuthamni lugha na utamaduni wa Taifa lao .

“Wengi wanaamini kuzungumza lugha ngeni ndiyo kuwa na lakini ni zaidi ya lugha yenyewe na  unajua shule zetu za siku hizi mtoto yuko darasa la kwanza haongei Kiswahili na sisi hatupigi vita lugha hizo tunasema ni lugha muhimu lakini tukumbuke sisi ni kisiwa hakuna nchi iliyounganisha watu wake wakazungumza lugha moja tuwe watendaji katika hili,”alieleza Prof.Mutembei.

Naye Mhadhiri wa Tafsiri na Taaluma  za Kiswahili  kutoka Chuo Kikuu Huria, Dk.Hadija Jilala alieleza kwamba endapo Serikali itapitisha lugha hiyo kutumika kama lugha ya kufundishia kuanzia  shule za masingi hadi vyuo vikuu itakuwa fursa ya kipekee katika kukuza Kiswahili.

“Kutakuwa na mafanikio makubwa sana shida ni kuhofia yajayo suala la ufundishaji na utafsiri vinaenda sambamba kwa sasa tunatumia kiingereza kufundisha na  unakuta mwalimu analazimika kuchanganya na kiswwahili ili wanafunzi waelewe hii itakuwa fursa kwetu watafsiri tuko tayari kutoa tafsiri ya vitabu vya kitaaluma zipo tafsiri nyingi tumezifanya kwa marejeleo ya kiingereza hakuna kinachoshindikana,”alisema Dk. Hadija.    

Aidha  akizungumzia ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu Oktavian Malaba ambaye ni mkalimani wa lugha ya alama alisema Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) lina jukumu la kuendeleza na kukuza lugha ya alama kama sehemu ya kutambua mchango wa watu wenye ulemavu kueneza Kiswahili.

“Changamoto kuwa ni kukubalika na kutambuliwa kwa ukalimani katika jamii tunasahau kuwa ni muihimu maana unaweza kukutana na mtu huyu utawasiliana naye vipi ikiwa hujui lugha yake tuwajali maana ni watu kama sisi wana uwezo wa kufanya makubwa kuliko hata wana  viungo kamili,”alieleza Mkalimani huyo. 

 


Post a Comment

0 Comments