IDARA YA VIJANA YAANZA KUSAJILI VIKOSI KAZI YA VIJANA.

 

📌FAUSTINE GIMU

IDARA ya vijana kanisa la Waadventista Wasabato kanda ya Dodoma imeanza kusajili vikosi kazi vya vijana  ndani ya kanisa kwa mwaka 2021 kwa ajili ya kazi za utume.

Akizungumza na   mtandao huu  alipotembelea kanisa la Waadventista Wasabato Chang’ombe  jijini Dodoma mratibu kiongozi idara ya huduma ya vijana kanisa la Waadventista Wasabato kanda ya  Dodoma  Mwinjilisti Mark Imori alisema lengo la kufanya  ziara katika makanisa mbalimbali ni kuhakikisha wanasajili vijana katika vikosi mbalimbali kwa lengo  kufanikisha kazi za utume pamoja na kutambulisha viongozi wa vikosi vya vijana.

Tupo mwanzo wa mwaka ambapo makanisa yote yapo katika usajili wa vijana hivyo na sisi kanda ya Dodoma tumeanza zoezi hili ikiwa ni pamoja na kutambulisha viongozi wa vijana
Mwinjilisti
 Imori.

 Aidha,Mwinjilisti Imori amesema  idara ya vijana inajiandaa na siku ya Matendo ya huruma duniani ambapo kanda ya Dodoma itafanyika  Ikulu ya Chamwino siku ya kilele Machi,20,2021 .

Kwa upande wake mratibu idara ya vijana kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa Kizota  Dodoma  Edwin Tongora alizungumzia sifa za kiongozi wa kikosi kazi cha vijana kanisani ni pamoja na mwenye juhudi na kusimamia mipango na kuhakikisha vijana wanaeneza utume.

Adam Rugazama ni miongoni mwa vijana kutoka kanisa la Waadventista Wasabato Chang'ombe jijini Dodoma ambapo alisema ni wajibu kwa kila kijana kujitoa katika kufanya kazi  ya utume.

Pamoja na kusajili vijana,idara ya vijana kanisa la Waadventista Wasabato kanda ya Dodoma  pia imeendelea kutoa mafunzo mbalimbali kwa vijana ikiwemo masomo ya ujasiriamali ,uchumba na ndoa ,kaya na familia huku ikitambulisha viongozi wasimamizi wa vijana [Master Guard] kwa mwaka 2021.

Wakati huohuo,Wazazi na Walezi ndani ya kanisa la Waadventista Wasabato wameaswa kuendelea kutimiza wajibu wa kuwafundisha na kuwaelekeza vijana    namna nzuri ya Kuendeleza kazi za utume.

Wito  huo ulitolewa na mratibu wa vijana kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa Kikuyu jijini Dodoma  mwinjilisti Demetrius Mapesi katika uzinduzi wa  huduma ya vijana Kanisa la Waadventista Wasabato Ntyuka  mtaa a Kikuyu ambapo alisema ni muhimu kuwajengea msingi mzuri vijana katika ukuaji wa kanisa.

Tutakuwa na kanisa lenye ustawi  mkubwa endapo  endapo vijana   watafundishwa miongozo mizuri ya kulitumikia kanisa tuwatie moyo

Aidha,Mwinjilisti Mapesi ametumia fursa hiyo kuwaasa vijana kuwa wa mfano kwa kufanya matendo mema ndani na nje ya kanisa ili kuondokana na dhana ya kudharauliwa.

“Ili ujana wako uheshimiwe  lazima ujichunge, uwe na heshima ,upendo ,waefeso  6:4 “alisema.

Hata  hivyo alitumia fursa hiyo kuzungumzia changamoto zinazowakabili vijana ikiwa ni pamoja na kutosikilizwa,kutopewa nafasi,majibu mabaya, pamoja na kuwa na matabaka hivyo  si vyema kudharau vijana  ,Timotheo 1:10.

Kwa upande wake Mzee wa Kanisa la Waadventista Wasabato Ntyuka Stephen Chacha alisema matarajio ya kanisa ni kuwalea vijana katika misingi bora ya kumtumikia Mungu.

Nao baadhi ya vijana waliohudhuria katika Sabato hiyo ya vijana akiwemo Yohana Asheri,Belenice Jackson na Japhet Paul walisema vijana ni nguzo muhimu kwa maendeleo ya kanisa  huku wakiwasihi vijana wengine kujiunga kwenye idara ya vijana katika kufanya kazi za utume.

Idara ya vijana imeundwa na vyama vitano vilivyochini ya kanisa la Waadventista Wasabato  wakiwemo wavumbuzi miaka  4 hadi 9,watafuta njia miaka  10 hadi 15, mabalozi ,wanafunzi vyuoni  pamoja na vijana wakubwa.

Post a Comment

0 Comments