WAZIRI NDALICHAKO AWAONGOZA WAKAZI WA DODOMA KUUAGA MWILI HAYATI JOHN KIJAZI.



📌FAUSTINE GIMU

WAZIRI wa elimu Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amewaongoza wakazi wa Jiji la Dodoma kuuaga mwili wa aliyekuwa Katibu Mkuu kiongozi, John Kijazi kwenye hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH)

Akimzungumzia  Marehemu Kijazi, Profesa Ndalichako alisema alikuwa ni mtu mpole, mnyenyekevu,mtulivu mchapakazi na  mzalendo aliyekuwaanafanya kazi yake kwa mujibu wa sheria.

 Kwa upande wake Katibu Mkuu Ikulu, Moses Kusiluka amesema ibada ya kiserikali ya kumuaga  Marehemu Balozi Kijazi itafanyika kesho  Jijini Dar es Salaam kwenye ukumbi wa Karimjee ambapo Rais John Magufuli atawaongoza wakazi wa  Dar   Es Salaam  kuuaga mwili huo kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Wilayani Korogwe mkoani Tanga kwa  mazishi yatakayofanyika kesho kutwa.

Naye Makamu  mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma, (UDOM) Profesa Faustine Bee amesema alikuwa anatamani kuendelea kufanya kazi na Balozi Kijazi kwani hata katika changamoto nyingi za chuo hicho walikuwa pamoja katika mapambano ambapo  haki ,wajibu na unatawala vilidumu  katika kupelekea  watanzania  kukimbilia chuo kikuu cha Dodoma  kusoma na kufanya kazi.



Mkuu wa mkoa wa Dodoma Dkt.Binilith Mahenge amesema Marehemu Balozi Kijazi katika kipindi cha uhai wake alikuwa mstari wa mbele katika harakati ya serikali kuhamia Dodoma huku Mkurugenzi wa hospitali ya Rufaa ya Benjamin Mkapa Dkt.Alphonce Chandika akizungumzia utii wake wakati akipata matibabu hospitalini hapo.

Balozi  Kijazi aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo  katika hospitali hiyo Jijini Dodoma  alipokuwa amelazwa kwa matibabu anatarajia kuzikwa siku ya Jumamosi,nyumbani kwao Wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga.

Balozi John Kijazi Agost,2020 aliteuliwa kuwa mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma kutokana na aliyekuwa Mkuu wa Chuo  hicho Benjamin William Mkapa kufariki Dunia.

 

Post a Comment

0 Comments