MWILI WA HAYATI DKT.MAGUFULI WAAGWA DODOMA,MAMA SAMIA ATOA NENO



📌 MWANDISHI WETU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akitoa Heshima za Mwisho kwenye jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Awamu ya tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma

Akihutubia wakati wa shughuli ya kitaifa kuaga mwili wa Magufuli kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma,  Rais Samia ametoa hofu wenye mashaka kuhusu uongozi wake akisema yuko tayari na anao uwezo mkubwa wa kuliongoza taifa. 

Rais Samia amesema licha ya yeye kuwa ni mwanamke, yuko imara na kwamba amepita kwenye mikono ya hayati Magufuli na hivyo amejifunza mengi kwa sababu alikuwa sio mtu wa kuyumbishwa na mwenye msimamo thabiti kwa kile alichoamini kina maslahi kwa Watanzania na kwamba yeye ataliongoza taifa bila mashaka yoyote. 

 

Kwa wale ambao wana mashaka mwanamke huyu ataweza kuongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nataka niwambie huyu aliyesimama hapa ni rais, wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambaye maumbile yake ni  mwanamke

 Rais Samia Suluhus Hassan

Aidha amesema yeye pamoja na viongozi wenzake wako tayari kuiendeleza miradi yote iliyoanzishwa na serikali chini ya uongozi wa Magufuli.

                                                        ANGALIA KWENYE CPC TV

                                                                              👇👇👇



Post a Comment

0 Comments