SPIKA NDUGAI: KUNA NYANI WANAFURAHIA KIFO CHA MWENYE SHAMBA

 


📌MWANDISHI WETU

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai amesema kuna baadhi ya watu wanafurahia kifo cha Dkt.Jonh Pombe Magufuli kitu ambacho si sahihi.

Akiongea kwa kutumia mfano wa ‘Nyani na Mwenye Shamba’ Spika Ndugai amesema wapo baadhi ya watu wanafurahia kuondoka kwa kiongozi huyu huku wakisahau kwamba kuna kesho ambayo uchapakazi wa Dk.Magufuli unahitajika.

Akizungumza na Wabunge pamoja na wafanyakazi wa Bunge wakati wa halfa ya kuaga mwili wa Dkt.Magufuli katika viwanja vya Bunge,Spika Ndugai  alisema utawala wake (Dkt.Magufuli) ni kama maisha mpanzi yaliyoelezewa katika biblia.

Kuna hadithi ya wale nyani waliokuwa wanakula shamba la mkulima kila linapostawi,lakini walipopata taarifa ya mwenye shamba kufariki wakafurahi sana na kula kila kilichopo shambani hapo,najua hata hapa kwetu wapo hao nyani.Mwaka unaofuata wakaenda tenda shamba lakini wakakuta shamba jeupe,wamesahau kuwa aliyekuwa anapanda ni Yule waliofurahia kifo chake.




Hata hivyo Spika Ndugai amesema mbegu ambayo hayati Dkt.John Pombe Magufuli aliyoipanda imedondoka katika udongo wenye rutuba na itamea kwa ustawi wa vizazi na vizazi  ni kama maisha mpanzi yaliyoelezewa katika biblia.

Amesema katika utawala wake Rais Magufuli amefanya mambo mengi ambayo kwake ilikuwa ni sehemu ya kutimiza ndoto yake ya kuifanya Tanzania bora.

“Naamini mbegu uliyopanda imedondoka katika udongo mzuri,umepanda barabara za lami,umepanda madaraja ambayo hatukuamini kama tungeyaweza,umepanda mbegu watanzania tutaendelea kuikuza mbegu hiyo.”

Spika Ndugai amesema licha ya kuwa kuna mengi ambayo dkt.Magufuli aliyafanya katika uhai wake,amesema yapo ambayo hayaonekani lakini yamebadilisha uelekeo wa taifa ikiwemo kupinga rushwa katika maisha ya mtanzania.

Mbunge wa Momba Mhe Condesta Sichalwe akilia kwa uchungu baada ya kuaga mwili wa Hayati Dkt.John Magufuli katika viwanja vya Bunge.


Ndugai pia amewakumbusha Wabunge hao kupitia hotuba ya mwisho ya Rais Magufulia aliyoisoma Bungeni hapo mnamo November 20,2020 ambayo alikuwa anatoa mtazamo wake wa miaka mitano ijayo,spika amesema hotuba ile ni wosia kwa bunge.

Pamoja na hilo Ndugai ameitaka viongozi wa serikali kuenzi ndoto  ya Dkt.Magufuli kuifanya Dodoma kuwa makao makuu kwa kuendeleza miradi yote ambayo marehemu aliianzisha ili kupendezesha jiji la Dodoma.

Aliposema Dodoma iwe makao makuu  nilimuuliza sasa itakuwaje Mungu akikuchuka,nilimshauri tutunge sheria.Tukatunga sheria na tukaipitisha hapa Bungeni hivyo Dodoma itaendelea kuwa makao makuu hilo lazima tulibebe.

Kwa upande wake Waziri Mkuu Kassim aliwataka wabunge hao kuenzi mambo makubwa ambayo Dkt.Magufuli ameyafanya katika majimbo yao na kama kuna miradi ambayo haijakamilika basi ikamilike kwa haraka ili kutatua kero za wananchi.



Pia Majaliwa aliwataka watanzania kuiombea familia ya Dkt.Magufuli kwa kuwa inapitia katika wakati mgumu.

“Ikiwa hii leo amelala hapa,mama yake yupo kitandani kwa miaka miwili sasa.Tumuombee pia mama ili aweze kuinuka kitandani.” Alisema Majaliwa na kusababisha vilio kutoka kwa miongoni mwa wabunge.

Hata hivyo Waziri Mkuu ametangaza mabadiliko katika kutoa heshima za mwisho kwa Dkt.Magufuli ikiwemo kuzungushwa kwa jeneza hilo katika barabara maarufu katika miji iliyobaki badala ya kulifungua kama ilivyofanyika katika mkoa wa Dar es Salaam.

Matamanio ya watu katika kumuaga Rais wao yamekuwa makubwa hivyo hatutoweza kumpitisha kila mmoja kuona,tuzungusha jeneza katika mitaa na barabara maarufu tu ili tuende na muda.


Awali, Naibu spika  Tulia Ackson aliamsha vilio miongoni mwa wabunge  baada ya kutoa hotuba iliyojaa huzuni na simanzi huku akimuelezea Dkt.Magufuli kama ngazi yake kufika katika nafasi aliyopo sasa.

“Mtu huyu amejua kutenda mema kwa taifa, JPM ametenda mema ambayo kila mtu ameyaona,wapo wanaobeza lakini mimi ni shahidi kwa kile alichopangiwa kutenda.” Alianza Dkt.Tulia

Akikariri kifungu cha kutoka kwenye biblia (Yacob 4:17) kwamba Rais Magufuli ametenda mema kwa sehemu yake ya alichotakiwa kufanya na muda wake wa kuondoka duniani baada ya kutimiza andiko hilo umefika.

Pia Dkt.Tulia amewataka wabunge kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan kwa vile pia alichaguliwa  kwa kura nyingi kama alivyochaguliwa Rais Magufuli.



Musa alipofariki kabla ya wanaIsraeli kabla hawajafika Kanaani,Mungu alizungumza na Joshua na kumtaka kuwa hodari na moyo wa kishujaa,Mama Samia ndiyo Joshua wetu atatufikisha kanani salama tumuunge mkono.

Dkt.Tulia.

                                                       ANGALIA KWENYE CPC TV
                                                                               ðŸ‘‡ðŸ‘‡ðŸ‘‡
                                                                            


Post a Comment

0 Comments