MAJALIWA:SIKU 21 ZA MAOMBOLEZO YAHAYATI MAGUFULI KUHITIMISHWA LEO.

 

📌FAUSTINE GIMU GALAFONI

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ametangaza kuisha kwa siku 21 za maombolezo ya msiba wa  hayati Rais.Dk John Magufuli na kwamba shughuli za Serikali zitaanza rasmi kesho.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  ameitoa kauli hiyo leo Jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa Habari  huku akisema Serikali itahakikisha inasimamaia muelekeo  wa utendaji kazi kama alivyoagiza Rais Samia suluhu Hassan na kuwataka watendaji wote kutimiza majukumu yao ipasavyo.



Hata hivyo amesema wataendelea kutekeleza malengo ya maendeleo ya ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi CCM hasa miradi mbalimbali ambayo imeanishwa katika ilani hiyo.

 

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu ametoa shukrani za pekee kwa vyombo vya  Habari nchini na kuahidi kutoa ushirikiano.

Ikumbukwe kuwa Hayati Dk John Magufuli alifariki dunia Machi17 Mwaka huu katika hospitali ya Mzena Jijini Dar-es-Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu ambapo alizikwa Machi26 mwaka huu Wilayani Chato Mkoani Geita.

Post a Comment

0 Comments